Ticker

6/recent/ticker-posts

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI PROFESA SOSPETER MUHONGO AKUTANA NA BALOZI WA INDIA NCHINI SANDEEP ARYA.


 Balozi wa India Nchini, Sandeep Arya (kushoto) akibadilishana mawazo na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kulia) mara baada ya kuwasili ofisini kwake. Lengo la ziara ya balozi huyo lilikuwa ni kuelezea nia ya serikali ya India katika uwekezaji kwenye sekta ya gesi nchini.
 Balozi wa India Nchini, Sandeep Arya (kushoto) akisaini kitabu cha wageni. Kulia ni Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.
 Balozi wa India Nchini, Sandeep Arya akielezea uzoefu wa nchi ya India kwenye  uwekezaji wa uzalishaji umeme kwa kutumia  gesi asilia.
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo akiongoza kikao  na Balozi wa India Nchini, Sandeep Arya pamoja na watendaji kutoka  Wizara ya Nishati na Madini, Shirika la  Umeme Nchini (TANESCO), Shirika la Maendeleo ya  Petroli Nchini (TPDC), Mamlaka ya Udhibiti wa  Huduma za Nishati na Maji Nchini(EWURA) na  Mamlaka ya Udhibiti wa Shughuli za Mkondo wa Juu wa Mafuta (PURA).
 Sehemu ya watendaji kutoka  Wizara ya Nishati na Madini wakifuatilia maelezo yaliyokuwa yanatolewa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (hayupo pichani)
 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo akisisitiza jambo katika kikao hicho.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa India Nchini, Sandeep Arya (kushoto).

Post a Comment

0 Comments