Ticker

6/recent/ticker-posts

TRA WAVUKA MALENGO YA UKUSANYAJI MAPATO ARUSHA

Image result for Apili  Mbaruku meneja wa tra arusha
meneja wa Mamlaka
ya mapato  (TRA) mkoani Arusha, bwana Apili Mbaruku.
Mamalaka ya mapato mkoa wa Arusha (TRA) imekusanya shilingi bilioni 64.6, ikiwa imevuka malengo
yake iliyojiwekea awali ya kuweza kukusanya shilingi bilioni 63.1.


Ongezeko hilo, ni sawa na asilimia 102, kulingana na meneja wa Mamlaka
ya mapato  (TRA) mkoani Arusha, bwana Apili Mbaruku.


Akizungumza katika mahojiano maalumu na mwandishi wa habari meneja wa mamlaka hiyo mkoa wa Arusha Apili  Mbaruku
alielezea kuwa ongezeko hilo linatokana na majumuisho ya makusanyo ya
mwezi Julai na Agosti mwaka huu.


“Ni kweli tumeweza kukusanya kiasi hichi cha fedha, nahii inatokana na
kukua kwa mwamko wa ulipaji kodi mkoani hapa  japokuwa bado zipo
changamoto kadhaa za baadhi ya wafanyabisahara kutokuelewa umuhimu wa
kulipa kodi,” alisema meneja huyo.


Apili ametaja sekta ya utalii kuongoza katika ulipaji huo wa kodi.

“Tumekuwa tukitoa elimu kwa wafanyabiashara waweze kuelewa umuhimu wa
kulipa kodi na kukwepa usumbufu usio na lazima,” alishauri meneja
huyo.


Hata hivyo, Mbaruku aliweka wazi kuwa ofisi yake ilishindwa kufikia
malengo ya ukusanyi wa mapato kwa mwaka wa fedha 2015/16.

“Kwa mwaka uliopita malengo yetu yalikuwa kukusanya shilingi 329.5
lakini kwa bahati mbaya tulipata shilingi bilioni 324.6 tu”.

Na Woinde Shizza,Arusha
Akifanunua zaidi kuhusu makusanyo ya mwaka huu,  Mbaruku alisema kuwa
kiasi cha bilioni 30.3  zilitokana na makusanyo ya ndani wakati
shilingi bilioni sita zilitokana na malipo ya ushuru.


Aidha, Mbaruku ameongeza kuwa ofisi yake inatarajia kukutana na
maofisa wa jiji la Arusha kuanza kukusanya makusanyo ya kodi za
majengo.


Kulingana na meneja  huyo wa TRA, ofisi yake inalenga kukusanya kodi
kutoka kwenye majengo 20, 536 mkoani hapa. Mamlaka ya mapato mkoni
Arusha(TRA) imevuka lengo la makusanyo yake kwa mwaka wa fedha
2016/17.


“Nia yetu ni kuanza kukusanya kodi kutoka kwenye majengo hayo, na
tayari tumeshafanya mawasiliano na maofisa wa jiji na kuweza
kubainisha majengo hayo,” aliongeza meneja huyo wa TRA mkoani Arusha.

Post a Comment

0 Comments