Ticker

6/recent/ticker-posts

WASHIRIKI WA SHINDANO LA MISS TANZANIA WATUA ARUSHA ,WAANZA ZIARA YA SIKU TATU KWA KUTEMBELEA OFISI ZA THE GUARDIAN /NIPASHE

Warembo 30 wanaoshiriki kinyanganyiro cha kumsala Miss Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja mara tu baada ya kutembelea ofisi za gazeti la Guardian zilizopo ndani ya mkoa wa Arusha
 picha ikionyesha baadhi ya warembo akiwemo mwenyeji wao ambaye ni miss Arusha wa pili kulia Maurine Ayubu wakiwa  ndani ya ofisi za gazeti la Gurdian na Nipashe zilizopo jiji Arusha
  Msimamizi wa kituo cha Gazeti la  Gurdian  na Nipashe mkoa wa Arusha na Manyara  Edward Qorro akiwa anatoa maelekezo mafupi kwa warembo juu ya kazi zinazofanya na magazeti hayo katika mkoa huu

 warembo ndani ya ofisi

 Msimamizi wa kituo cha Gazeti la  Gurdian  na Nipashe mkoa wa Arusha na Manyara  Edward Qorro akipokea mkoa wa Shukrani kutoka kwa Mshiriki wa mashindano ya miss Tanzania kutoka mkoa wa Arusha Maurine Ayubu ambaye pia ndio mshindi wa Miss kanda ya kaskazini mara baada yakumaliza kutmbelea ofisi za magazeti hayo zilizopo apa Arusha

 mkuu wa kituo siaakaamua kutumia mda huo kuji selfie na warembo

 Meneja masoko wa gazeti la Gurdiaan   Swalehe Walii akiwa anatoa zawadi ya soda kwa mrembo Maurine Ayubu ambaye ni mwenyeji wa warembo wenzake wanaoshiriki shindano hilo kwani ametokea mkoa wa Arusha





 warembo wakiwa wanatoka katika ofisi za gazeti la  The gurdian mara baada ya kumaliza kutembelea
 nili
 nilipata wasaa wa kupiga picha na baadhi ya wakuu wa msafara wa warembo hao wa kwanza kabisa ni kulia mimi mwenyewe mmiliki wa blog ya libenele la kaskazini woinde shizza akifuatia akifuatiwa Mshiriki wa mashindano ya miss Tanzania kutoka mkoa wa Arusha Maurine Ayubu ambaye pia ndio mshindi wa Miss kanda ya kaskazini,wa pili kushoto ni muuandaaji wa  shindano la mss kanda ya mashariki Alex NIkitas

warembo wakitoka ndani ya ofisi za The Gardian na nipashe zilizopo mkoani Arusha

 Habari picha na Woinde Shizza,Arusha
Jumla ya warembo 30  kutoka mikoa mbalimbali  hapa nchi ni wanashiriki shindano la kumsaka mrembo wa Tanzania (Miss Tanzania) leo wameingia Rasmi mkoani Arusha na kutembelea ofisi za gazeti la The Guardian na Nipashe  ikiwa ni moja ya kazi ambazo watazifanya wakiwa mkoani hapa.

Akizumza na waandishi wa habari  Mkuu wa Itifaki wa Miss Tanzania Albert Makoye alisema kuwa wameingia jijini hapa leo na wanakaa kwa muda wa siku tatu ,na katika siku hizo wanampango wa kufanya shughuli mbalimbali za kijamii

Aidha alisema kuwa pia ndani ya siku hizo tatu kutakuwa nashindano la Top model ambalo litafanyika Jumamosi October 15 katika ukumbi wa Triple A ulipo ndani ya jiji la Arusha 

"tunafanya shindano hilo katika ukumbi wa triple A natunarajia wananchi wengi wa Arusha watajitokeza kuwaona warembo hawa na kiingilio cha shindano hilo ni shilingi 10000 tu hivyo napenda kutumia mda huu kuwaalika wananchi wa Arusha kuja kumuangalia nani atakuwa Top Model"alisema Makoye

Alisema kuwa  mbali na hapa warembo hao wameshatembelea mikoa mbalimbali ikiwemo Mkoa wa Dodoma,Singinda ,Dar  es Salaam  hapa Arusha na hatimaye wanatarajia kuondoka na kwenda mwanza ambapo ndipo shindano hili linafayanyika kwa mwaka huu .

Alisema kuwa shindano la Miss Tanzania linatarajiwa kufanyika october 29 katika ukumbi wa Rock City Mall  ambapo alibainisha adi sasa warembo wote 30 wapo vizuri na wanasubiria siku yenye ifike na maandalizi yashindano yamekamila

Kwa upande wake mkuu wa kituoa cha The Gardian /Nipashe mkoa wa Arusha na Manyara Edward Qorro alitoa shukrani kwa warembo hao kuwatambelea na kuwatakia kila la kheri katika mashandano hayo wanayotarajia kushiriki hivi karibuni
 



Post a Comment

0 Comments