Ticker

6/recent/ticker-posts

DC KASESELA MAZOEZI LAZIMA IRINGA ILI KUJENGA UCHUMI

Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akiwa kwenye mazoezi na wananchi wa kijiji cha Tosamaganga pamoja na mwanachama wa club ya Tosamaganga sports club 
Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela akicheza Mpira wa kikapu kuashiria kuwa anapenda Mpira wa kikapu

Na Fredy Mgunda,Iringa


Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela aliwaomba wananchi kuendelea kufanya mazoezi kwa ajili ya kuimalisha afya zao pamoja kuujenga uchumi wa nchi hii.

Tukiendelea kufanya mazoezi tutapunguza sana kupata magonjwa mbalimbali kwa kuwa tuna kuwa tunaimalisha afya na kujenga miili yetu lakini hii itasababisa wananchi kujituma kufanya kazi kwa nguvu na morali mpya kila mwanzo mwa wiki kwa kuwa wanakuwa na nguv,stamina na akili Mpya kutokana mazoezi ya mwisho mwa Juma.

"Kwa mfano mimi saizi nipo sawa kiakili kutokana na haya mazoezi maana bila haya mazoezi nisinge kuwa vizuri kiaafya,saizi naweza kufanya kazi kwa masaa mengi kutokana na hili zoezi la Leo sasa nawaomba wananchi na viongozi mbalimbali kufanya mazoezi ili kuongeza ufanisi kazini"alisema Kasesela

Aidha Kasesela aliwashukuru wananchi wa Tosamaganga sports club kwa kuanziasha club ya Tosamaganga ambayo inamichezo mingi kama mpira wa miguu,mpira wa pete,riadha,na mpira wa kikapu hivyo naomba wananchi wengine waanzishe vitu kama hivi ili Wilaya nzima iwe inafanya mazoezi kwa kuimalisha Afya.

Kasesela amewataka viongozi wa kata,kijiji,mtaa,na tarafa kuanzisha mazoezi huku waliko ili kupanua wigo wa eneo kubwa la watu kufanya mazoezi ili kuimalisha afya zao na kupunguza kunyemelewa na magonjwa mbalimbali ambayo yamekuwa yanapunguza nguvu kazi za taifa katika kujenga uchumi wa taifa.

"Hii ni moja ya club ambayo nimeizindua ambayo itatuongezea wigo wa sehemu za kufanyia mazoezi ya kuimalisha afya zetu na kuipa moyo serikali kupanua wigo wa maeneo ya kuafanyia mazoezi" alisema Kasesela

Nao baadhi ya viongozi wa club ya Tosamaganga sports club walimushukuru mkuu wa Wilaya kwa kukuza Michezo katika Wilaya ya Iringa na kuongeza ufanisi wa kazi hasa makazini kwa kuwa ndio jadi ya kukuza uchumi katika mkoa wa Iringa.

Post a Comment

0 Comments