Kesi ya ugaidi inayowakabili watuhumiwa 61 ikiwemo ya ulipuaji wa mabomu maeneo mbalimbali Jijini Arusha
Imeendelea kutikisa mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Arusha ambako kwa siku ya leo ni watuhumiwa 9 pekee wameweza kufika mahakamani
Imeendelea kutikisa mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Arusha ambako kwa siku ya leo ni watuhumiwa 9 pekee wameweza kufika mahakamani
Kwa taarifa iliyotolewa na mwakilishi wa uongozi wa magereza mbele ya hakimu mkazi Gwantwa Meankuga alidai kati ya watuhumiwa 61 wa kesi za ugaidi ni watuhumiwa 9 pekee walioweza kufika mahakamani siku ya leo
Alisema watuhumiwa hao wameendelea kusisitiza kutofika mahakamani mpaka pale watakapoambiwa upelelezi umekamilika
Pia wakati huo huo wakili wa jamhuri Penina Johackim aliomba mahakamani impangie tarehe nyingine kutokana na upelelezi kutokamilika
Hata hivyo,Kaimu Hakimu mkazi Gwantwa Mwankuga alisema kesi hiyo itasikilizwa tena tarehe 25 mwezi aprili
Nimekuwekea majina ya watuhumiwa 9 waliofika mahakamani leo hapo chini.
1. Shaban Idd,
2. Yusuph Ally
3. Sumalya Juma,
4. Kimolo Suleiman
5. Abdallah Juma,
6. Bahan Lazaro
7. Sadick Hussein,
8. Masumau Fadhil
9. Abrahman
Picha 5 kutoka nje ya mahakamani leo watuhumiwa wakiwasili na kuondoka mahakamani hapo.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia