Ticker

6/recent/ticker-posts

UJUE MMEA WA GUGU KAROTI UNAOENEA NCHINI KWA KASI TAMBUA NA ATHARI ZAKE



Mmea wa gugu karoti ambapo unamadhara katika ngozi ya mwanadamu ,ukigusana na ngozi unatoka mapele pamoja na ngozi kuharibika.


Mwandishi Wa habari Wa kituo cha Luninga cha Star TV Jijini Arusha Angelo Mwoleka  aking'oa gugu karoti akiwa amevaa mfuko mweusi mkononi kuepuka jani hilo lisimguse kwenye ngozi.
Waandishi Wa habari kutoka katika vyombo mbalimbali vya habari Jijini Arusha wakiwa katika eneo ambalo gugu Karoti limeota wakiwa wamevaa vifaa mkononi kwaajili ya kung'oa .





Mkurugenzi Wa Taasisi ya ECHO  inayojishughulisha na utafiti Wa kilimo na kupunguza njaa ndugu Erwin Kinsey ,akitoea elimu kwa waandishi Wa habari juu ya gugu katoti


Mwanamazingira Travis Silvens akiwa anawaonyesha waandishi Wa habari gugu karoti kama anavyoonekana


Mtaalamu Wa kilimo kutoka Taasisi ya ECHO ,Charles Bonaventure akiwa anatoa elimu kwa waandishi Wa habari juu ya gugu karoti.


Dr.GirAus Page   ambaye amejitolea kwa aendeleo ya kimataifa kutoka nchini Australia,ambaye anafanya kazi na  Taasisi ya ECHO .



Waandishi Wa habari wakifuatilia mafunzo yanayoendele .
Waandishi Wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya Jijini Arusha wakifuatilia mada
Mwandishi Wa habari kutoka gazeti la The Guardian Edward Qorro akitoa shukrani kwa niaba ya waandishi
Waandishi wakiwa katika Picha ya Pamoja na watoa elimu juu ya gugu Karoti

Kufuatia tishio la mmea hatari unaofahamika kwajina la gugu karoti (Partheniun hysterophorus)kwa afya za binadamu,mifugo na mazingira waandishi wa habari mkoa wa Arusha wamepewa elimu kuhusu mmea huo na kutakiwa kuielimisha jamii kuhusu mmea huo.

Mmea huo wenye madhara kwa binadamu mazao ya mashambani Pamoja na mifugo umesambaa maeneo mengi nchi ikiwemo Arusha ,Kilimanjaro ,Manyara na Kilimanjaro 

Asili ya mmea huo umetokea nchini Mexico ,uligundulika  miaka ya 1960 ambapo mmea mmoja unauwezo wa kuzaa mbegu 25,000  kwa mche mmoja.

Aidha mmea huo watu wengine  wamekua wakiutumia katika shughuli za upambaji , wanatumia kama ufagio, wameyapalilia kama maua majumbani ambapo madhara yake kupata muwasho na vipele mwili nzima.

Mnyama akila majani hayo anaweza kufa maziwa yake yanakuwa machungu yenye uchachu  na yanaleta madhara kwa mtumiaji,kwa kuku haiwezi kuendelea kutaga tena.

Post a Comment

0 Comments