Na Woinde Shizza, Arusha
Kesi ya kughushi nyaraka
na kujifanya Afisa usalama wa Taifa,inayomkabili mwenyekiti wa uvccm mkoa wa
Arusha,Lengai Ole Sabaya imeshindwa kuendelea Mara baada ya upande wa Mashtaka
kudai haina nia ya kuendelea na shauri hilo.
Akizungumza mahakamani
hapo mbele ya hakimu Gwanta Mwankuga,Wakili wa serikali Grace Madikenya alisema
kuwa jamhuri kupitia kifungu namba 91 cha mwenendo wa makosa ya jinai haina nia
na shauri hilo kutokana na shahidi wake muhimu kwenda masomoni nje ya nchi.
"Mheshimiwa hakimu
upande wa jamhuri haina nia ya kuendelea na shauri hilo chini ya kifungu namba
91 cha mwenendo wa makosa ya jinai"Alisema wakili wa serikali
Hata hivyo Wakili wa
upande wa mshitakiwa,Grace Mndeme na Charles Abrahamu waliweka pingamizi
juu ya hoja hiyo walidai kuwa Wakili wa serikali wanania ya kuichezea mahakama
na wanalengo la kumtesa mteja wao.
" Mheshimiwa sisi
tunapinga hoja iliyoletwa mbele yako na Wakili msomi wa serikali kwa sababu
upande wa jamhuri wanaitumia vibaya mahakama na wanania ya kumtesa
mshitakiwa,na si Mara yao ya kwanza kufanya hivyo"Alisema Mndeme
Alieleza kuwa hoja ya
wakili wa serikali haina nia njema na mshitakiwa kwani sio Mara ya kwanza
kueleza nia ya kutoendelea na shauri hilo na baadae mtuhumiwa anapoachiwa
hukamatwa na kulazwa mahabusu na baadae kufikishwa mahakama na kushitakiwa kwa
shauri hilo hilo.
Pia aliieleza mahakama
hiyo kuwa kumekuwepo na uzembe katika uendeshaji wa shauri hilo unaofanywa na
Mwanasheria wa serikali ,kwa sababu wakati kesi hiyo inaendelea walishindwa
kuleta mashahidi badala yake walikimbilia kuliondoa shauri hilo mahakamani.
Baada ya kuwepo kwa
pingamizi hilo kutoka kwa mawakili wa mshitakiwa ,hakimu Mwankuga aliahirisha
shauri hilo kwa Madai kuwa atatoa uamuzi Mdogo siku ya Ijumaa ,Mai 28 mwaka
huu.
Akizungumza nje ya
mahakama mshitakiwa, Sabaya alieleza kukerwa na hatua ya upande wa serikali
kuendelea kupiga danadana kesi yake alidai kuwa kuna mpango wa kuendelea
kumdhalilisha kwani yeye ni mwanasiasa aliyechaguliwa na wananchi anahitaji
kuwatumikia
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia