Na Woinde Shizza,Arusha
Wananchi
wametakiwa kuhakikisha wanakula nyama ambazo zimechinjiwa katika
machinjio zinazotambulika kiserikali na zilizopimwa nawataalam wa mifugo
ili kuweza kuepuka magonjwa ya milipuko yanayotokana Na nyama.
Hayo
yamebainishwa jana na Meneja wa machinjio ya Jiji la Arusha (Arusha
Meet)Fabian Kisingi wakati akiongea na waandishi wa Habari ambapo
alisema Kumekuwa na magonjwa mengi sana ambayo yanawakumba ng'ombe akiwa
ajachinjwa na hata ndani ya nyama baada ya kuchinjwa iwapo ngombe
hatari pimwa na wataalam kunauwezekano mkubwa binadamu akila nyama ile
ikamzuru .
Alisema
kuwa kumekuwepo na magonjwa ambayo yanapatikana ndani ya nyama kama
vile Kimeta ,Rifitivale na mengine mengi ambapo pasipo kupimwa na
watalaam wa mifugo wanaotambulika Na waliosomea maswala ya mifugo ni
ngumu mtu wa kawaida kutambua magonjwa hayo.
"ngoja
nitoe mfano kuna baadhi ya maini yanakutwa Na wadudu na sio rahisi mtu
wa kawaida kutambua wadudu hao kwani ni wadogo sana sasa ,watalaam wetu
wakipima ndio wanatambua na tukishatambua basis tunachukuwa maini Yale
na kwenda kuyateketeza mbali maana maini Yale hayafai kuliwa hata na
mbwa" alisema Fabian
Aidha
aliwataka wananchi wote wanaochinja ng'ombe zao mitaani kuacha Mara
moja maana ni hatari sana kwani huko mitaani akuna mtaalam ambaye
anaweza kutambua kama mnyama huyo ni mzima anamaradhi au sio mzima
"Nichukue
fursa hii kuwasihi wananchi kuhakikisha wanachinja mifugo yao mahali
panapotambulika kisheria Na palipo na watalaam, sehemu ambayo ukaguzi
unafanyika vizuri sehemu ambayo wanaakikisha wanawapa watu nyama nzuri
isiyo Na magonjwa Na inayofaa kwa binadamu" alisema Fabian
Kwa
upande wake Meneja uzalishaji wa machinjio ya Arusha Meet Happy
Ignatius Ngowi alisema kuwa kumekuwepo Na tatizo la wananchi kupeleka
ng'ombe zenye mimba kuchinjwa kitu ambacho sio kizuri Na pia ni kibaya
kwani kuchwa kule kwa ng'ombe wale kunahatarisha kupoteza uzao mdogo wa
ng'ombe.
Alisema
kuwa pamoja wananchi wanaona ng'ombe ni wengi lakini kwa wingi huu wa
ng'ombe wajawazito wanavyoletwa kuchinjwa kunahatarisha kupoteza uazazi
mdogo kwani ng'ombe hawa wengi wanaoonekana kuwepo ambao ni wakubwa kuna
ambao wanazeeka na wengine wanakula hivyo iwapo tukiligungia macho hili
itafika mahali tutakosa ng'ombe wa kuchinja kabisa
Aliitaka
serikali kukemea vikali sana uchinjwaji wa ng'ombe ambao wanamimba Ili
kuweza kuendelea kulinda kizazi hichi cha watoto wa dogo .
Meneja WA machinjio ya Arusha Meet Fabian Kisingi akiiongea Na Mwandishi wa habari
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia