Taifa hilo linakumbwa na matatizo makubwa ya kisiasa ambayo yamechangia kuzorota kwa usalama nchini humo.
Muhula wa mwisho madarakani kwa rais Joseph Kabila, ulimalizika mapema mwezi huu, lakini uchaguzi mkuu umeahirishwa.
Wakati
huohuo mapigano makali yalishuhudiwa hii leo kati ya vikosi kutoka
jeshi la Jamuhuri ya kidemkrasia ya Congo FARDC, na waasi wa kikundi cha
Maimai katika kijiji cha Moikene yapata kilomita sitini kusini mwaa
mji wa Beni katika mkoa wa kivu ya kaskazini mashariki mwa DRC.
Duru za kuaminika zaeleza kuwa waasi wa Mai-Mai walishambulia ngome moja
ya jeshi la congo FARDC mapema alfajiri na kuanza kurushiana risasi.
Walioshudia
mapigano hayo wanasema kuwa yalichukuwa mda wa saa tano lakini hakuna
anayejua idadi ya waliouawa wala kujeruhiwa.
Tangu mwanzo wa
mwezi Oktoba mwaka wa elfu mbili na kumi na nne Beni ,imekuwa shamba la
vita pamoja na mauaji, huku raia wa kawaida wakiathiriwa vibaya.
Kundi la waasi wa ADF kutoka nchini Uganda ndio linatajwa kuwa tishio kubwa katika maeneo hayo.
Licha
ya majeshi ya serikali kujitahidi kukabiliana na wapiganaji kutoka
makundi ya waasi ya ADF pamoja na Maimai, Hali ya usalama bado ni tete
Beni.
Makundi hayo yamekuwa yakitekeleza mashambulizi ya mara kwa
mara dhidi ya wanavijiji, ambapo wahalifu huwavamia na kuanza kuwauwa
kwa kutumia shoka ,mapanga pamoja na bunduki na kusababisha vifo vingi.
Maelfu ya wanavijiji pia wamelazimishwa kuhama makwao.
Hata hivyo jitihada za kupata maoni ya upande wa serekali pamoja na jeshi kuzungumzia mauaji hayo hapa Beni ziliambulia patupu.
CHANZO:BBC
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia