Kutokana na Taarifa za Raia nane wa Tanzania kukamatwa nchini Malawi
kwa kwa kile kinachodaiwa kuwa ni ujasusi nchini humo Serikali ya
Tanzania Kupitia waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika
Mashariki Balozi Dokta Augustino Mahiga amesema juhudi za kumaliza
suala hilo linaendelea.
Akizungumza jijini Arusha Waziri Mahiga amesema Serikali ya Tanzania
imeshachukua hatua za kumaliza suala hilo ikiwemo kuzungumza na serikali
ya ya Malawi.
Kuhusu Suala la mgogoro wa Ziwa Nyasa, Balozi Maige ameseama jitihada
za kuukwamua zinaendela chini ya kamati Maalumu iliyoundwa kwaajili ya
kutatua suala hilo
Watanzania 8 wanaodaiwa kuwa ni majasusi wa Serikali ya Tanzania
walikamatwa kamatwa nchini Malawi mwaka jana kwa tuhuma za kuingia
kwenye mgodi wa urani wa Kayerekera uliopo nchini humo kinyume cha
sheria.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia