Ticker

6/recent/ticker-posts

KINANA ASHIRIKI MAZISHI YA KATIBU WA UVCCM


Na Mwandiishi Wetu,kilimanjaro
Katibu mkuu wa CCM Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana leo ameshiriiki mazishi ya aliyekuwa Katibu wa Hamasa,Sera,Utafiti na Mawasiliano  katika tawi la Shiirikisho la Chuo Kikuu cha Tiba KCMC marehemu Edwin Christopher Msele aliyefariki katika ajali ya gari huko Mwika wilayani Rombo Mkoanii hapa.
Kinana ameongoza  mamia ya wananchi,wana ccm,wana chuo,wana familia,ndugu  jamaa na marafiki kushiriki mazishi yaliofanyika katika kijiji cha Kitandu kata ya Okaoni wilaya ya Moshi vijijini mkoani kiliamnjaro .
Akiwaslisha salamu za Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungwana  wa Tanzania Dk John Magufuli ,CCM na jumuiya zake, Kinana alisema kwa hakika CCM imepokea kwa masikitiko, huzuni na fazaa  taarifa za kifo cha  mwanachama huyo.
Alisema marehemu Edwin Msele alikuwa kiongozi wa mstari wa mbele katika chama kupitia  jumuiya ya uvccm na kwamba amepoteza maisha wakati chama na jumuiya ya vijana ya ccm ikimtegemea na kumuamini.
"Edwin katika uhai wake alitenga muda wake wa kushughulikia na kujibidiisha n amasomo kwa  kujiendeleza kitaaluma pia alikuwa na matarajio ya kushiriki siasa huku akionyesha uzalendo wa kulitumikia Taifa lake" Alisema Kinana.
Aidha katibu mkuu huyo wa ccm alisema ccm na Taifa limempoteza mtu aliyeandaliwa kitaaluma kwa ajili ya kulitumikia Taifa na watu wake kwani alikuwa mwanafunzi wa mwaka wa nne akichukua fani ya utabibu katika chuo kikuu cha kcmc.
"Kwaniaba ya Mwenyekiti wa ccm Dk johnMagufuli,chama cha mapinduzi na jumuiya zakenawasIkisha salamu za mkono wa pole na rambirambi kwa wazazi,familia ,ndugu na jamaa kutokanana msiba huo ulioacha majonzi na huzuni"AlielezaKinana.
Pia Kinana katika msiba huyo amewasilisha mchango wa mkono wa pole wa ccm na jumuiya zake wakati huku akiwasihi wazazi na familia ya marehemu Edwin Msele kuwa na mioyo ya subira na ustahamilivu katika kipindi hiiki kigumu cha msiba na maombolezo.
Hata hivyo katibu mkuub huyo wa ccm alisema vifo vya wanachama wanne vijana walikuwa na sifa za uchamungu,kupenda elimu na kwamba walI bar ikiwa kuwa na  vipawa na vipaji vilivyohiitaajika katika jamii.
"Vijana hawa hawatoki katika familia zenye majina makubwa au familia zenye uwezo mkubwa,ni vijana waliosimama kwa kwa uwezo na miguu yao ,mishumaa yao ya uhai  imezimika,mungu akifunga  mlango mmoja atafungua mingine"Alisema Kinana
Katika mazishi hayo kinana aliambatana na waziri wa maliasili na utalii Profesa Jumanne Maghembe, Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro Sadiq Mecky said,Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka,Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro Idd Juma na Mkuu wa wilaya ya Moshi Kipi Warioba.

Post a Comment

0 Comments