Ticker

6/recent/ticker-posts

WAZIRI KAIRUKI AZINDUA RASMI, OFISI YA RAIS –UTUMISHI NA UTAWALA BORA ILIYOPO MAKAO MAKUU YA NCHI DODOMA


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akizungumza na Vyombo vya Habari kabla ya kuzindua rasmi utoaji wa huduma wa ofisi yake iliyopo Makao Makuu ya Nchi Dodoma. Wengine ni baadhi ya Watumishi wa ofisi hiyo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akikata utepe kuzindua rasmi ofisi yake iliyopo Makao Makuu ya Nchi Dodoma. Wanaoshuhudia ni watumishi wa ofisi hiyo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akizungumza na Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Sera, Bw. Mathias Kabunduguru mara baada ya kuzindua rasmi huduma za ofisi hiyo.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Prof. Idris Kikula akisaini kitabu cha wageni ofisini kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) mara baada ya kumtembelea waziri huyo ofisini kwake. Wanaoshuhudia ni baadhi ya waandishi wa habari na watumishi wa ofisi hiyo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akijionea moja ya shubaka linalotumika kutunzia majalada katika masijala ya ofisi yake, mara baada ya kuzindua utoaji wa huduma wa ofisi hiyo iliyopo Makao Makuu ya Nchi Dodoma. Wanaoshuhudia ni baadhi ya watumishi wa ofisi hiyo na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Prof. Idris Kikula.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa ofisi yake iliyopo Makao Makuu ya Nchi Dodoma, mara baada ya kuzindua rasmi utoaji wa huduma wa ofisi hiyo. Aliyejumuika nao ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Prof. Idris Kikula (Wapili kutoka kulia).
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Prof. Idris Kikula akizungumza na Vyombo vya Habari mara baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) kuzindua rasmi ofisi yake iliyopo katika jengo la Kitivo cha Sanaa na Sayansi Jamii lililopo Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Muonekano halisi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora iliyopo katika jengo la Kitivo cha Sanaa na Sayansi Jamii Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), mara baada ya ofisi hiyo kuzinduliwa rasmi na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb).

Post a Comment

0 Comments