Mhe,Jaji Mstaafu wa mahakama kuu kanda ya Arusha Fatuma Hamis Masengi |
Picha ya pamoja kati ya waheshimiwa majaji kanda ya
Arusha na Kilimanjaro ,Wakwanza kulia ni mhe,Jaji Dkt.Modesta
Opiyo,Wakwanza kushosto ni mhe,Jaji Salma Maghimbi,akifuatiwa na
aliyeko kushoto kwake mhe,Jaji Sekela Mushi,akifuatiwa na mhe,Jaji
mstaafu Fatuma Hamis Masengi wakiwa na majaji wengine pamoja na
waheshimiwa mahakamu.
Mhe,Jaji Mstaafu wa mahakama kuu kanda ya Arusha Fatuma
Hamis Masengi akiwa na waheshimiwa mahakimu wa mahakama ya
mwanzo(waheshimiwa mahakimu hao wamelelewa na mhe,Fatuma
Masengi)
Picha ya pamoja ya waheshimiwa majaji pamoja na mawakili wa serikali,na wale wa kujitegemea.
Sherehe
za kumuaga aliyekuwa Jaji mfawidhi wa mahakam kuu kanda ya Arusha
Mhe,Fatuma Hamis Masengi ,zimefanyika leo katika mahakama kuu
ya ndanda hiyo na kuhudhuriwa na wageni mbalimbali wakiwemo
majaji,mahakimu,mawakili wasajili wa mahama watendaji pamoja na wageni
waalikwa.
Sherehe
hizo zimeanza majira ya saa asubuhi katika mahakama ya wazi
ambapo Jaji Fatuma alianza kufanya kazi mnamo mwaka 1974 katika
mahakama ya mwanzo na
kuendelea kuitumikia mahakama hadi alipoteuliwa kuwa jaji mfawidhi
mahakama kuu.
Amewataka
majaji na mahakimu pamoja na wale wote wanaofanya kazi za kimahakama
wafanye kazi kwa kumtegemea Mungu huku wakijua kazi yeyote ina
changamoto zake hivyo ni vyema kufanya kazi kwa weledi zaidi na kwa
kuzingatia sheria inavyosema,wakimtendea haki kila mtu kwa stahiki.
Amewataka
wanawake kutokukata tamaa huku akisema kuwa wanawake wanaweza kuliko
wanaume japo kuwa wakati mwingine wanaume wanaona kama vile wanawake ni
wanyonge lakini mwanamke anaweza pale ambapo anasimama kwa nafasi yake
na kulitumikia kusudi kwa wakati na weledi.
"Wanawake
wenzangu msikate tamaa na kujiona wewe ni dhaifu ,tunaweza msibweteke
unapopata nafasi itumie vizuri bila kuaharibu taratibu zilizowekwa
,fanya kazi kwa bidii na jamii itaona juhudi zako ,wanawake tunaweza
"alisema masengi.
Aidha
Jaji Fatuma amesema kuwa anamshukuru sana Mungu kwa kumuwezesha
kwa wakati wote ambapo amekuwa akifanya kazi yenye
majukumu mazito, amezishukuru Asasi za kiserikali na zile
zisizo za kiserikali,amewashukuru wale wote walioshirikiana nae katika
kipindi chote alichokuwa akitimiza majukumu yake ya
kikazi.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia