Ticker

6/recent/ticker-posts

USHIRIKA WAHIMIZA VIJANA KUWEZESHWA NCHINI


Na Mwandishi Wetu,Kiliamnjaro
Kanisa la kilutheri usharika wa Masma limeshauri na kuzihimiza mamlaka zilizoshika madaraka ya utawala kuwalenga na kuwaibua vijana wenye upeo,maono na bidii ya kufanya kazi kwa lengo la kujitegemea.
Pia kanisa hilo limesema vijana ambao hushinda  toka asubuhi hadi usiku wakiwa kwenye,unywaji viroba na uzurururaji hawataweza kuondokana na kadhia hatari ya ujinga,umasikini na maradhi.
Mchungaji Andrew Munisi aliitoa matamshi hayo leo wakati wa aibada ya kuiuombea maiti ya marehemu Anord Jonathan Swai ibada iliofanyika katika usharika wa kanisa la kilutheri la Masama wilayani Hai mkoani hapa.
Alisema ni  jukumu la serikali kuwapatia nyenzo na uwezeshaji utakaofaa ili vijana walioko hivi sasa katika karakana za ufundi,viwanda vidogovidogo na ujasiriiamali  wapate mwanga zaidi wa kujituma na kufanyakazi.
Akimzungumzia marehemu Anord,Mchungaji Munisi alimtaja kuwa ni mfano bora miongoni mwa vijana waliokuwa upeo,maono na maarifa ya kujituma pia kuitumikia jamii alioishi nayo.
"Tuna kundi kubwa la vijana nchini wenye maono,upeo na dhati ya kujitoa na kujituma,wanahitaji kusaidiwa na kuwezeshwa ili wajikwamue, tukiwataza huku wakibaki vilabuni, kunywa viroba na kuzurura,watapotea "Alisema.
Hata hivyo mchungaji huyo aliwahimiza waumini kuendelea kumuabudu mungu,kumtegemea na kila mja apime umri wake na jinsi anavyomtumikia mungu wake.
"Pamoja na Anord kuwa mwanasiasa bado alikataa siasa za chuki,upasi na mgawanyiko,alitenda mambo kwa wakati huku akimtumikia mungu wake,chama ,kazi na wazazi wake"Alieleza mchungaji Munisi
Mchungaji huyo wa kanisa la kilutheri  alisema kumtumikia mungu lazima kuambatane na umri wa binadamu katika, maisha yake duniani kwasababu umri hukimbia mno na mungu atawahukumu wale  waliotenda dhambi.
"Kama tunauhitaji ufalme wa mbinguni  hatutaupata mpaka mtu atamapozaliwa mara ya pili,hata farisayo,tajiri na mjumbe wa baraza kuu la mayahudi Nicodem alipotaka kujua ufalme wa mbinguni Yesu alimjjbu amapaka mtu azaliwe mara ya pili"Alisema Mchungaji Munisi.
Anord Swai aliyekuwa Mwenyekiti wa uvccm wilaya ya Hai mkoani hapa amezikwakwa heshima zote katika kijiji alichozakiwa huko Mweera kata ya Masama kati wilaya ya Hai mkoani hapa.

Post a Comment

0 Comments