CHONGOLO -LAZIMA IPATIKANE SULUHU YA KUDUMU UVAMIZI WA TEMBO KWENYE MAKAZI YA WATU

 


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) komredi Daniel Chongolo, ameendelea kutoa msisitizo kwa Wizara ya Maliasili na Utalii kushughulikia Tembo Wavamizi wa mazao ya Wananchi mkoani Simiyu.

Ametoa kauli hiyo leo June 02, 2022 wakati alipowasili katika Wilaya Itilima mkoani Simiyu ukiwa ni muendelezo wa ziara yake yenye lengo la kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025 katika mikoa ya Shinyanga na Simiyu.

Akizungumza katika kata ya Nkoma, komredi Chongolo amesema Wizara ya maliasili na Utalii ni lazima ihakikishe inaleta Suluhu ya kudumu kukomesha Changamoto ya Uvamizi wa Tembo kwenye Mashamba na Makazi ya Wananchi.

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

Previous Post Next Post