FILAMU YA TANZANIA ROYAL TOUR YAANZA KUZAA MATUNDA

 

Mkurugenzi wa Masoko katika Kamisheni ya Utalii Zanzibar Mohamed Mansour  wa pili kushoto akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wenzake wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar katika banda lao lililopo katika maonyesho ya karibu Kili fear yanayoendelea mkoani Arusha


Na Woinde Shizza , ARUSHA 

Filamu ya Tanzania  Royal Tour iliochezwa na Rais Samia imeanza kuonyesha mafanikio mara baada ya wageni kuanza kuingia hapa nchini na kutembelea vivutio mbalimbali vilivyopo hapa nchi

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Masoko katika Kamisheni ya Utalii Zanzibar Mohamed Mansour  alipokuwa akiongea na waandishi wa habari katika banda lao lililopo katika maonyesho ya karibu Kili fear 2022 yanayofanyika katika viwanja vya kisongo vilivyopo ndani ya halmashauri ya Jiji la Arusha ambapo alimpongeza Rais Samia Kwa kuandaa filamu hiyo ambayo alisema imesaidia sana kutangaza nchi pamoja na Vivutio vilivyopo 

Alisema kuwa tangu kuzinduliwa kwa filamu ya Royal Tour kumekuwepo na ongezeko la watalii kutembelea nchi yetu  Kwa ajili ya kuja kuona vivutio mbalimbali vilivyopo ,ambapo pia alibainisha kuwa anaamini jinsi filamu hiyo itavyoendelea kuonyeshwa itawavutia wageni wengi ambao ni watalii na hata wawekezaji kwani katika filamu hiyo Rais Samia ameweza kuonyesha vivutio mbalimbali ,pamoja na fursa ambazo zinapatikana katika nchi yetu.

"Nimpongeze Rais Kwa kitendo alichokifanya Cha ubunifu ambao umeshirikisha pande zote mbili yaani Zanzibar na huku,ameonyesha ninamna gani wanaendelea  kuimarisha muungano  ,maana hata katika filamu hiyo Rais Samia ameweza hata kumshirikisha Rais wa Zanzibar   ili nayeye aweze kuonyesha baadhi ya vivutio vinavyopatikana  Zanzibar na kutangaza fursa zilizopo"alibainisha Mohamed 




Alisema kuwa filamu hii ni mkombozi kwa nchi yetu kwa sababu  kwa muda mrefu tumekuwa tukihangaika kwa kutafuta majukwaa ya kimataifa ya namna gani ya kutangaza vivutio vya utalii. 

Alibainisha kuwa filamu hiyo imekuwa  mkombozi haswa katika kipindi hichi ambapo mataifa mbalimbali ikiwemo Tanzania zinahaha kujikwamua kiuchumi baada ya janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19. 


Akiongelea maonyesho haya alisema wameamua kushiriki ili kuweza kutangaza vivutio mbalimbali vinavyopatikana  Zanzibar ikiwemo chumba kilichojegwa ndani ya bahari huko Pemba , shughuli za uvuvi zinazofanywa  ,mji mkogwe pamoja na tamaduni mbalimbali zinazopatikana humo

Alisema maonyesho haya ni mazuri na uanasaidia sana kujitangaza kwani watu kutoka nchi mbalimbali wanashiri pia yamesaidia kukutanisha nchi zote za afrika mashariki kwani zikiwemo Kenya ,uganda ,Burundi ,Rwanda na wenyeji Tanzania ambapo alisema nchi ambayo haijashiriki ni Kongo lakini anaamini itashiriki katika  maonyesho ya miaka ijayo

Aidha alimalizia Kwa kuwataka watanzania kutembelea vifutio vya utalii vilivyopo hapa nchini kwani masharti yaliyokuwepo awali yamepungua huku alibainisha kuwa wameamua kuungana na Tanzania katika maonyesho haya ili kuunga mkono jitiada za kutangaza  filamu ya Tanzania Royal Tour.





Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

Previous Post Next Post