Ticker

6/recent/ticker-posts

D.C,POLISI WAPEKUA NYUMBA YA MFANYABIASHARA ARUSHA

Mkuu wa wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma,Dan  Makanga kwa kushirikiana na baadhi ya askari wa kitengo cha upelelezi cha jeshi la polisi mkoani Arusha wamedaiwa kuingia na kisha kupekua  nyumba na ofisi ya mfanyabiashara wa utalii jijini Arusha,Mathew Mollel wakipekua hati ya kiwanja aliyodai kutapeliwa kiongozi huyo.

Tukio hilo lililovuta hisia za watu wengi  jijini hapa hivi karibuni jijini Arusha limedai kwamba mkuu huyo wa wilaya aliongozana na askari hao wawili hadi katika ofisi ya mfanyabiashara huyo iliyopo jengo la hoteli ya New Safari ambapo mbali na upekuzi huo alidaiwa kuwamuru wavunje safe ya mfanyabiashara huyo kwa lengo la kupekua hati ya kiwanja.

Tayari jeshi la polisi kupitia kwa mkuu wa upelelezi mkoani Arusha,(RCO) Duwani Nyanda limekiri kutokea kwa tukio hilo ambapo juzi wakati akihojiwa na gazeti hili alisema kuwa ni kweli askari hao walitumwa kupekua nyumba na ofisi hizo   kwa kuwa mfanyabiashara huyo anakabiliwa na kesi ya kughushi na kisha  kujipatia mali kwa njia ya udanganyifu.

“Ni kweli nilituma vijana wangu na huyo mtu ana kesi ya kughushi na kujipatia mali kwa njia ya udanganyifu “alisema Nyanda

Haahivyo,alipoulizwa kuhusu madai ya Makanga kuwaamuru askari wake kuvunja safe ya mtuhumiwa huyo Nyanda alikwepa kuzungumzia suala hilo lakini alijibu kwa kifupi”Kwani kuna ubaya akiwepo? alikuwa ana identify(anahakiki) mali zake zilizoibiwa”.

Akihojiwa na gazeti hili,Mollel ambaye pia ni Mkurugenzi wa kampuni ya Raimbow Tours and Shuttle alidai kuwa mnamo Agosti 21 mwaka huu askari wawili waliwasili katika ofisi yake na kumtaka kufika katika ofisi ya mkuu wa idara ya upelelezi mkoani Arusha kwa madai anakabiliwa mashtaka mbalimbali.

Mollel,kwa huzuni alidai kuwa aliitikia wito huo na kisha ambapo aliwasili katika ofisi hiyo na kisha kumkuta Makanga akiwa na baadhi ya askari ambapo alisimulia kwamba alinyang”anywa simu zake mbili za mkononi na askari hao ambapo walimtaka kutowasiliana mtu yoyote.

Hatahivyo,alisema kuwa mnamo Agosti 22 mwaka huu  aliwasili tena katika ofisi hiyo na kisha kuamriwa kuelekea katika ofisi yake ambapo waliongozana na askari hao wawili,Makanga pamoja na mtu mmoja aliyemtambua kwa jina moja la Shija ambapo mara baada ya kuwasili katika ofisi hiyo walianza kufanya upekuzi wa hati hiyo.

“Baada ya kupekua kila sehemu mheshimiwa mkuu wa wilaya aliwaambia askari wavunje safe ili kuipekua hati hiyo lakini niliwaambia funguzo ziko nyumbani ndipo tukaongozana hadi Mianzini nyumbani kwangu wakaanza kupekua hadi chumbani”alisimulia Mollel
 
Mollel,alidai kuwa mara baada ya kufanikiwa kuchukua nyaraka hizo ndipo alipofanikiwa kuwasiliana na wakili wake aliyemtaja kwa jina la Duncan Ooola na walifika tena katika ofisi ya upelelezi mkoa ambapo alikabidhi hati hiyo ambayo hadi sasa inashikiliwa na ofisi hiyo na kudai ameamriwa kuripoti kila jumatano ya wiki.

Kwa mujibu wa maelezo ya Mollel alisimulia kuwa chanzo cha mgogoro huo ni kwamba mamo 1997 Makanga alimpatia kiwanja hicho kwa makubaliano ya kujenga nyumba ya kuishi na familia yake ambapo na pindi atakafanikiwa kupata sehemu nyingine atalazimika kukiachia kiwanja hicho  lakini mwaka 2007 alimua kutafuta hati ya kiwanja hicho kwa kuhofia eneo hilo kumegwa na wakala wa barabara nchini(Tanroads) mkoani Arusha.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Kasulu(Makanga) alipohojiwa kwa njia ya simu juzi alikiri kuwa jijini Arusha tarehe ya tukio  na kudai alishiriki hatua kwa hatua kwa kuwa alikuwa anahakiki mali zake alizodai kutapeliwa na mfanyabiashara huyo.

Hatahivyo,Makanga alikanusha vikali madai ya kuwaamuru askari hao wavunje safe la mtuhumiwa huyo huku akisisitiza kuwa alifanikiwa kuipata hati hiyo ambayo hatahivyo alidai ilibadilishwa jina kiujanja.

“Ni kweli nilikuwa Arusha hii ni kesi kubwa nilikuwepo kwenye tukio ili kushuhudia mali zangu lakini sikuamuru ivunjwe safe  kwani tulifanikiwa kuipata hiyo hati”alisema Makanga

Tukio hilo linatajwa kuzivuruga familia mbili za Mollel na Makanga huku ikielezwa ya kwamba watu hao wameoa  katika familia moja wilayani Bariadi mkoani Shinyanga

Post a Comment

0 Comments