Ticker

6/recent/ticker-posts

WASHINDI WA TUZO ZA HABARI ZA TANAPA WATEMBELEA KIJIJI CHA UTALII WA UTAMADUNI AFRIKA KUSINI CHA LESEDI


   Mshindi wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013 Gerald Kitabu (The Guardian) akisalimiana na kijana wa Kizulu katika kijiji cha Utamaduni cha Lesedi walipotembelea ili kujifunza utalii wa kiutamaduni nchini Afrika Kusini.

  Mshindi wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013 Vedasto Msungu (ITV) akisalimiana na kijana wa Kizulu katika kijiji cha Utamaduni cha Lesedi walipotembelea ili kujifunza utalii wa kiutamaduni nchini Afrika Kusini.

  Katika Utamaduni wa Kizulu boma hulindwa na mlinzi anayekaa juu kwa ajili ya kuangalia waingia na watokao kama anavyoshuhudiwa hapa alipotembelewa na Washindi wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013 nchini Afrika Kusini.

Washindi wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013 kutoka kulia Gerald Kitabu, David Rwenyagira na Vedasto Msungu wakifurahi pamoja na wanakijiji cha Wazulu cha Lesedi walipowatembelea ili kujifunza utamaduni

  Mshindi wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013 David Rwenyagira (Radio Five) akishika ngao kwa ajili ya kujikinga na adui ambao ni mojawapo ya utamaduni wa Wazulu.

   Washindi wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013 wakiendelea kupata somo juu ya tamaduni mbalimbali zinaopatikana  nchini Afrika Kusini.

  Washindi wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013 katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Kituo cha Utamaduni cha Lesedi, Afrika Kusini.

   Lugha ya Kiswahili nayo yafahamika vema Afrika Kusini kama inavyoonekana hapa katika picha iliyopigwa na Washindi wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013.

Post a Comment

0 Comments