
Fedha kiasi cha shilingi milioni 500 zilizotolewa na Serikali kwa
ajili ya kuendeleza kituo kituo cha afya Usa – River kwa lengo la
kuboresha huduma za afya na kuondoa vifo vya mama namtoto
ujenzi na uboreshaji wa kituo hicho unaendelea mpaka sasa shughuli
zilizofanyika ni ujenzi wa Majengo ya maabara na nyumba ya Mtumishi
yaliyofikia hatua ya upanuzi pamoja na ujenzi wa ukamilishaji wa misingi
ya majengo mengine unaendelea kuwa na ubora
mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa kituo hicho cha Afya Allen M.
Mwenda ambaye ni miongoni mwa wakilishi 11 wa wananchi wa Kata ya Usa
–River waliopo kwenye kamati mbalimbali za uboreshaji wa kituo hicho
amesema wanaridhishwa na ujenzi unaoendelea kwani changamoto iliyokuwepo
ni ya vifaa na kwa sasa vifaa vyote vinavyohitajika vipo na mafundi
wanaendelea na ujenzi wa amefafanua kuwa ujenzi na uboreshaji wa kituo
hicho umekua fursa ya ajira kwa vijana ,wanawake na wananchi wengine
hivyo nguvu kazi ipo ya kutosha.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Christopher J.
Kazeri amesema kutokana na usimamizi na ufuatiliaji wakaribu wa ujenzi
wa kituo hicho cha Afya Usa-River kwa kuhakikisha vifaa vyote
vinavyohitajika kwenye ujenzi huo vinapatikana kwa wakati sambamba na
nguvu kazi wanatarajia ujenzi huo kukamilika mapema kabla ya tarehe ya
ukomo iliyotolewa ambayo ni tarehe 31 Mai 2017.
Aidha Mkurugenzi Kazeri amewahimiza wataalamu wanaosimamia ujenzi huo
kuzingatia ubora kwa kueleza kua lengo la kutumia Force Account ni
kupunguza gharama,kuondoa urasimu na kuarakisha ujenzi huo kukamilika
mapema .
Allen M. Mwenda ambaye ni miongoni mwa wakilishi 11 wa wananchi wa
Kata ya Usa –River waliopo kwenye kamati mbalimbali za ujenzi na
uboreshaji wa kituo hicho,amesema yeye kama mwenyekiti wa kamati ya
ujenzi pamoja na wajumbe wanaridhishwa na ujenzi unaoendelea na
kufafanua kua ‘’changamoto iliyokuwepo ni ya vifaa na kwa sasa vifaa
vyote vinavyohitajika vipo na mafundi wanaendelea na ujenzi pia nguvu
kazi ipo kwani ujenzi wa kituo hicho umekua fursa ya ajira kwa vijana
,wanawake na wananchi wengine .
Mmoja wa wataalamu wanaosimamia ujenzi na uboreshaji wa kituo hicho
Philipo Paulo ambaye ni fundi sanifu wa majengo amethibishisha ujenzi wa
Majengo ya maabara na nyumba ya Mtumishi yaliyofikia hatua ya upanuzi
pamoja na ujenzi wa ukamilishaji wa misingi ya majengo mengine
unaendelea kuwa na ubora
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Christopher J. Kazeri
alipotembeleamesema kutokana na usimamizi na ufuatiliaji wakaribu
kwenye ujenzi wa kituo hicho wataalamu wanaosimamia ujenzi huo
kuhakikisha wanazingatia ubora kwa kila hatua ya ujenzi huo.





(wakwanza kushoto)Mkurugenzi Mtendaji wa
halmashauri ya Wilaya ya Meru Christopher J. Kazeri akiteta jambo juu ya
ubora wa ujenzi wa msingi wa jengo la jengo la kuhifadhia maiti,