Mwenyekiti wa Baraza la Mamlaka ya Mji Mdogo Ngaramtoni mheshimiwa
Elias Munis ameonesha matumaini makubwa juu ya upatikanaji wa huduma ya
Maji kwa wananchi na wakazi wa Mamlaka hiyo na vitongoji vyake ifikapo
mwishoni mwa mwaka huu wa 2018.
Mwenyekiti huyo amesema hayo alipozungumza na mwandishi wetu mara
baada ya kufunga Mkutano wa Baraza la Mamlaka hiyo la kujadili taarifa
za utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo kwa kipindi cha robo ya pili kwa
mwaka wa fedha 2017/18 .
Mwenyekiti Munisi amesema kuwa Mamlaka inamatumaini makubwa kuwa
miradi ya maji inayotekelezwa katika mamlaka hiyo pindi itakapokamilika
itapunguza adha ya maji inayowakabili wananchi wa Mamlaka hiyo kwa muda
mrefu sasa.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia