mkuu wa mkoa Simiyu Antoni Mtaka akikabidhi makepteni wa Timu ya taifa ya
Riadha leo rasmi bendera ya Tanzania kwenda
kuwakilisha nchi katika mashindano ya mbio za nyika za dunia
yayotarajiwa kufanyika Marchi 26 nchini Uganda ,kapteni wa kike anaitwa Magdalena Krispini akiwa mkono wa kushoto ,na kapteni wa kiume Fabian Josephy akiwa mkono wa kushoto.
Riadha leo rasmi bendera ya Tanzania kwenda
kuwakilisha nchi katika mashindano ya mbio za nyika za dunia
yayotarajiwa kufanyika Marchi 26 nchini Uganda ,kapteni wa kike anaitwa Magdalena Krispini akiwa mkono wa kushoto ,na kapteni wa kiume Fabian Josephy akiwa mkono wa kushoto.
Na Woinde Shizza,Arusha
Timu ya
taifa ya Riadha leo imekabidhiwa rasmi kupeperusha
bendera ya Tanzania kwenda kuwakilisha
nchi katika mashindano ya mbio za nyika
za dunia yayotarajiwa kufanyika Marchi 26 nchini Uganda.
Akikabidhi
bendera hiyo , Rais wa shirikisho la Riadha Tanzania ambaye pia ni mkuu wa mkoa
wa Simiyu, Antony Mtaka alisema kuwa
mashindano haya ni makubwa kidunia na
nchi zipatazo 70 zitashiriki mashindano
haya ,pia kutakuwepo na nchi zingine 216 ambazo zitashiriki lakini hazitaleta
timu.
Aidha
alibainisha kuwa hii ni mara ya kwanza kwa nchi
ya Tanzania baada ya miaka 26 kupita kupeleka timu ambayo imekamilika
ikiwa na wachezaji 28 sawa na nchi zingine kama vile Ethiopia,Kenya na Uganda.
“Imepita
miaka 26 tangu nchi yetu ya Tanzania ikipeleka
wachezaji wakiwa kamili katika mashindano mbalimbali ,lakini kwa sasa hivi
naweza kujivunia kwakuwa tumewafua wachezaji vya kutosha na tumepata timu
kamili yenye wachezaji 28 ambao ni sawa na wenzetu wa Kenya na Ethiopia wanavyopelekaga
wachezaji ivyo tunaimani kabisa kwa wingi huu lazima tutashinda na medani
kurudi hapa nchini”alisema Mtaka
Alisema
kuwa mashindano hayo yanaitaji mchezaji
mwenyewe kuondoa tofauti alizonazo na kujituma zaidi kwani mbali na kuiwakilisha nchi lakini
pia akishinda itamsaidia yeye mwenyewe kujinufaisha kwani zawadi zinazotolewa
ni kubwa nazinamnufaisha mshindi.
Alisema kuwa
wachezaji wamekaa kambini kwa muda
mchache lakini wamejifua vya kutosha
hivyo anaimani kabisa wanapoenda kushindana watashinda .
“Napenda
kutumia muda huu kuwashukuru na kuwapongeza shirika la hifadhi ya Taifa (Tanapa)
kwa kudhamini safari nzima ,na napenda kuahidia fedha zao hazitapotea bure bali
zitawalipa pale wanariadha wetu watakapo rudi na medani ,napenda kuwaambia hakuna
mchezo mwingine ambao wanaweza kuutumia kujitangaza zaidi ya riadha”alisema
Mtaka
Kwa upande
wake kaimu mkurugenzi wa Tanapa Nyamakumbati
Mafuru alisema kuwa wao kama
Tanapa wameona michezo ni njia moja wapo na muhimu ya kutangaza utalii wetu wan chi yetu hivyo ndio maana tumeona tutumie fursa hii
iliyojitokeza
“Unajua
mashindano haya yanauthuriwa na watu wengi kutoka sehemu mbalimbali hivyo
tumeona ni njia moja wapo ambayo tutaitumia kutangaza vivutio vilivyopo katika
nchi yetu na ndio maana tumeamua kudhamini kuwapeleka timu hii ya taifa
Uganda ili wakatuwakileshe na
kututangaza pia “alisema Mafuru