Ticker

6/recent/ticker-posts

TANZANIA MISS SUPER MODEL KUFANYIKA MARCH 31 JIJINI ARUSHA

Shindano la kumsaka   Tanzania Miss super Model linatarajiwa kufanyika mapema mwezi marchi 31 mwaka huu katika ukumbi wa hotel ya Mounti Meru uliopo ndani ya jiji la Arusha 

Akiongea na waandishi wa habari muaandaaji wa  shindano hilo Ibra Thabit alisema maandalizi  yamekamilika na hadi sasa warembo wote wanaoshiriki shindano hilo wako kambini kwa ajili ya mazoezi 

Alisema kuwa  jumla ya warembo 14 kutoka mikoa yote ya Tanzania watashiriki shindano hili na mshindi atakae patikana ataenda kuwakilisha mashindano ya  Dunia Miss Top Super Model yanayotarajiwa kufanyika nchini china

 washiriki wa shindano la Tanzania Miss super Model wakiwa katika picha ya pamoja katika hotel moja   iliopo katika mji mdogo wa mererani wakati walipo fanya ziara katika mji huo


 mkurugenzi wa Mnyalu intatament  Charles Endru akiwa pamoja na warembo wa Tanzania miss super model

Post a Comment

0 Comments