Ticker

6/recent/ticker-posts

USIKU WA WANAWAKE WANAOFANYA KAZI MGODI WA DHAHABU ACACIA BULYANHULU KAHAMA


Hapa ni katika ukumbi wa Jensen Complex Hotel uliopo Kakola katika halmashauri ya Msalala wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga ambapo usiku wa Machi 08,2017 ,wanawake wanaofanya kazi mgodi wa dhahabu wa Acacia Bulyanhulu wamefanya hafla fupi ili kusherehekea siku ya wanawake duniani ambayo hufanyika kila mwaka tarehe 8 mwezi Machi.


Hafla hiyo imeambatana na utoaji zawadi kwa wanawake wanne shupavu mgodini lakini pia wanawake wote wanaofanya kazi mgodini wamepatiwa zawadi mbalimbali na Meneja Mkuu wa Mgodi wa Acacia Bulyanhulu,Graham Crew katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani.
Awali kabla ya kufanya hafla hiyo,wanawake hao walitoa zawadi ya shuka 140 kwa ajili ya kusaidia huduma za afya kwa akina mama katika vituo vya afya Bugarama na Lunguya ambapo pia walitoa zawadi ya sabuni,mafuta ya kujipaka na dawa za meno.
Wanawake hao wametumia fursa hiyo kuwataka wanawake wengine kujitokeza kufanya kazi katika migodi badala ya kuamini kuwa kazi za migodini ni kwa ajili ya wanaume tu.
Naye Meneja Mkuu wa Mgodi wa Acacia Bulyanhulu,Graham Crew alisema mgodi huo hivi sasa unafanya jitihada za kuwahamasisha akina mama kufanya kazi mgodini ili kuhakikisha kuwa wanafikia usawa wa kijinsia yaani 50 kwa 50.
Crew aliongeza kuwa hivi sasa wanawake wanashika nyadhifa za juu za uongozi hali inayoonesha wazi kuwa mgodi unajali wanawake.
Mwandishi mkuu wa Malunde1 blog,Kadama Malunde alikuwepo wakati wa hafla hiyo ametusogezea picha 43....Tazama hapa chini
Machi 8,2017 usiku-Mtaalamu wa Mawasiliano mgodi wa dhahabu wa Acacia Bulyanhulu,Mary Lupamba akimkaribisha Meneja mkuu wa mgodi huo Graham Crew
Meneja Mkuu wa Mgodi wa Acacia Bulyanhulu,Graham Crew akizungumza wakati wa hafla ya kuadhimisha siku ya wanawake duniani iliyokutanisha wanawake wanaofanya kazi katika mgodi huo unaokadiriwa kuajiri wanawake zaidi ya 100
Meneja Mkuu wa mgodi wa dhahabu wa Acacia Bulyanhulu Graham Crew akizungumza na wafanyakazi wanawake katika mgodi huo ambapo alisema hivi sasa wafanyakazi wanawake ni wachache sana ukilinganisha na idadi ya wanaume na kuongeza kuwa mgodi unafanya jitihada za kuhakikisha kuwa idadi ya wanawake inaongezeka ili kuwe na usawa wa 50 kwa 50 kwa wanaume na wanawake
Wafanyakazi wa mgodi wa Bulyanhulu wakipiga makofi wakati wakimsikiliza meneja mkuu wa mgodi huo
Meneja Mkuu wa mgodi wa dhahabu wa Acacia Bulyanhulu Graham Crew alisisitiza pia kuhusu umuhimu wa kuhamasisha elimu kwa watoto wa kike katika shule za msingi na sekondari kwani elimu ndiyo itaweza kubadilisha maisha yao
Wanawake wanaofanya kazi mgodi wa Bulyanhulu wakifurahia jambo
Meneja Mkuu wa mgodi wa dhahabu wa Acacia Bulyanhulu Graham Crew (kushoto) akiteta jambo na Meneja wa Ustawi wa Jamii na Kampuni ya Acacia Bulyanhulu,Elias Kasitila
Mjumbe wa serikali ya kijiji cha Kakola kata ya Kakola bi Apaikunda Nathan Palanjo akizungumza wakati wa maadhimisho hayo ya siku ya wanawake duniani ambapo aliushukuru mgodi huo kwa kuwasaidia akina mama katika vituo vya afya na kuwasaidia baiskeli wanafunzi wa shule ya sekondari Bugarama na Bulyanhulu
Meneja Mkuu wa mgodi wa Acacia Bulyanhulu Graham Crew (wa pili kulia) akiwa ameshikana mkono na viongozi mbalimbali kuonesha ishara ya umoja wakati wa maadhimisho hayo ya siku ya wanawake duniani.Wa kwanza kulia ni Meneja wa Ustawi wa Jamii na Kampuni ya Acacia Bulyanhulu,Elias Kasitila.Wa kwanza kushoto ni Meneja wa Usalama Acacia Bulyanhulu Terry Little akifuatiwa na mwalimu mkuu wa shule ya msingi Bulyanhulu 'A',Joyce Lwanji na Mjumbe wa serikali ya kijiji cha Kakola kata ya Kakola bi Apaikunda Nathan Palanjo
Wafanyakazi wa mgodi wa Acacia Bulyanhulu wakiwa wameshikana mkono kuonesha ishara ya umoja
Wafanyakazi wa mgodi wa Acacia Bulyanhulu wakicheza ukumbini
Wanawake wanaofanya kazi katika mgodi wa Acacia Bulyanhulu wakicheza muziki ukumbini.Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya Jamii mgodi wa Acacia Bulyanhulu Sarah Ezra Terry
Afisa Mahusiano wa Mgodi wa Acacia Bulyanhulu Zuwena Senkondo akizungumza ukumbini namna walivyoshiriki katika siku ya wanawake duniani kwa kutembelea vituo vya afya Bugarama na Lunguya na kutoa zawadi ya baiskeli katika shule ya sekondari Bulyanhulu na Bugarama
Meneja mkuu wa Mgodi wa Acacia Bulyanhulu Graham Crew( katikati) akijiandaa kukabidhi zawadi kwa wanawake wanne shupavu katika mgodi huo ambapo walipewa zawadi ya picha na shilingi 100,000/= kila mmoja
Meneja mkuu wa Mgodi wa Acacia Bulyanhulu Graham Crew akikabidhi zawadi ya picha kwa bi Sivirina baada ya kuonesha utendaji mzuri zaidi kutoka kitengo cha Mazingira.
Meneja mkuu wa Mgodi wa Acacia Bulyanhulu Graham Crew akikabidhi zawadi ya picha kwa mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya Jamii mgodi wa Bulyanhulu Sarah Ezra Terry 
Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya Jamii mgodi wa Acacia Bulyanhulu Sarah Ezra Terry ambaye anashikilia nafasi ya juu katika uongozi akipokea zawadi ya picha 
Meneja mkuu wa Mgodi wa Acacia Bulyanhulu Graham Crew akikabidhi zawadi ya picha kwa mwanamke mdogo kiumri Mwanaisha Moshi ambaye ameonekana kuwa mchapakazi zaidi
Meneja mkuu wa Mgodi wa Acacia Bulyanhulu Graham Crew na Meneja wa Ustawi wa Jamii na Kampuni ya Acacia Bulyanhulu,Elias Kasitila wakiwa wamejifunga mitandio ya akina mama baada ya kuwavalisha mitandio wanawake wanaofanya kazi mgodini kama sehemu ya zawadi ya meneja mkuu wa mgodi huo
Wanawake wanaofanya kazi mgodini wakiwa wamevaa mitandio waliyozawadiwa na Meneja mkuu wa Mgodi wa Acacia Bulyanhulu Graham Crew 
Meneja wa Ustawi wa Jamii na Kampuni ya Acacia Bulyanhulu,Elias Kasitila akicheza muziki na wanawake wanaofanya kazi mgodini
Meneja mkuu wa Mgodi wa Acacia Bulyanhulu Graham Crew akiangalia wafanyakazi wa mgodi huo wanavyocheza muziki
Muziki unaendelea
Mtaalamu wa Mawasiliano mgodi wa dhahabu wa Acacia Bulyanhulu,Mary Lupamba akicheza muziki
Muziki unaendelea
Akina mama wakicheza muziki
Meneja wa Usalama Acacia Bulyanhulu Terry Little akicheza muziki na Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya Jamii mgodi wa Acacia Bulyanhulu Sarah Ezra Terry
Muziki umekolea......
Muziki umenoga haswaaa....
Kushoto ni Maria na Sarah wakifungua shampen
Maria na Sarah wanafungua shampen
Maria na Sarah wameshafungua shampen
Wafanyakazi wa mgodi wa Acacia Bulyanhulu wakigonga cheers
Mjumbe wa serikali ya kijiji cha Kakola kata ya Kakola bi Apaikunda Nathan Palanjo akigonga cheers na Meneja wa Ustawi wa Jamii na Kampuni ya Acacia Bulyanhulu,Elias Kasitila.
Zoezi la kugonga cheers linaendelea
Cheers!!!!
Meneja mkuu wa mgodi wa Acacia Bulyanhulu Graham Crew akigonga cheers na wafanyakazi wake
Meneja wa Usalama mgodi wa Acacia Bulyanhulu Terry Little akigonga cheers na wanawake wanaofanya kazi mgodini
Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya Jamii mgodi wa Bulyanhulu Sarah Ezra Terry akiwa na furaha ukumbini 
Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya Jamii mgodi wa Bulyanhulu Sarah Ezra Terry na Meneja mkuu wa Mgodi wa Acacia Bulyanhulu Graham Crew
Picha ukumbini
Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya Jamii mgodi wa Bulyanhulu Sarah Ezra Terry akiwaasa wafanyakazi wenzake kufanya kazi kwa juhudi huku akieleza kuwa wanawake wana nafasi kubwa ya kushika uongozi mgodini
Kushoto ni Afisa Mahusiano wa Mgodi wa Acacia Bulyanhulu Zuwena Senkondo akibadilishana mawazo na wafanya kazi wenzake.

Post a Comment

0 Comments