Ticker

6/recent/ticker-posts

PAPA FRANCIS AANZA ZIARA RASMI NCHINI CHILE HUKU KUKIWA NA HALI YA WASIWASI

Papa Francis akiwa ziarani nchini Chile,Amerika ya kusini.



Papa Farancis ameanza ziara yake nchini Chile huku kukiwa na wasiwasi wa kutokea shambulizi,kufuatia tishio lililotolewa kupitia vipeperushi vilivyo tolewa katika shambulio la
awali kabla ya kuanza kwa ziara hiyo.
Kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki Dunian alipokelewa kwa shangwe na zaidi katika uwanja wa Santiago mji mkuu wa nchi hiyo,ambapo waumini wa kanisa Katoliki,viongozi mbali mbali wakiongozwa na rais wa Chile Michelle Bachelet walikuwepo pia.
Taifa la Chile lina zaidi ya asilimia 60 ya raia wake ni wakristo kati yao asilimia 45 ni wakatoliki,huku taifa hilo likiwa la pili katika bara la Amerika ya kusini kwa kuwa na idadi ya watu wasio na dini.
Hata hivyo ziara hii ya Papa nchini Chile imetanguliwa na matukio ya kushambuliwa kwa mabomu makanisa matatu mji mkuu wa taifa hilo Santiago huku washambuliaji wakiacha vipeperushi kwamba shambulio linalofuata ni dhidi ya Papa,kutokana na matukio hayo rais Bachelet amesema hayo ni matukio ya kushtusha.
Hii ni ziara yake ya kwanza nchini Chile tangu kuchaguliwa kwake,ziara hiyo ikikumbana na upinzani mkubwa kufuatia kashfa udhalilishaji wa kingono dhidi ya watoto unaodaiwa kufanywa na baadhi ya makaaisisi wa kanisa hilo nchini Chile.
Papa Francis leo anatarajiwa kukutana na waathirika wa ukatili wa kijeshi uliofanywa na dikteta Augusto Pinochet,ambapo pia zaidi ya nusu milion wanatarajiwa kuwa katika mkuasanyiko katika maeneo ambayo Papa atayatembelea katika ziara yake.Papa Francis amewasili nchini Chile ikiwa ni mwanzo wa ziara yake ya wiki moja nchini humo pamoja nan chi ya Peru.Sherehe za kumkaribisha Papa zimefanyika uwanja wa ndege wa Santiago.

Post a Comment

0 Comments