Na Woinde Shizza,Arusha
Tatizo la
tapia mlo kwa watoto chini ya miaka mitano na wanawake walio kwenye umri wa
kuzaa limepata ufumbuzi baada ya baada ya taasisi ya utafiti ya selian ilipo
mkoani Arusha kuja na suluhisho la maharage bora yenye wezo wa kupunguza tatizo
hilo
Akiongea na
waandishi wa habari wa kanda ya kaskazini wakati wa ziara ya kimafunzo ilioandaliwa Tume ya taifa ya sayansi Teknolojia na ubunifu (COSTECH) mtafiti kutoka kituo
cha utafiti cha Selian(SARI) kilichopo jijini Arusha Shida Nestory Mahenge alisema kuwa tatizo la watoto na wanawake
walio katika umri wa kuzaa ndio ulikuwa chachu ya upatikanaji wa mbegu za
maharage haya ambayo yana madini ya chuma pamoja na zinki
Maharage haya yenye
madini ya chuma na zinki yanazalishwa
katika hali ya kawaida ya kiagronomia aina hizi za maarage ya chuma na zinki ni
haya tuliyoyataja ya Selian14 pamoja na selian15 na maharage haya ni mazuri
kwani madini ya chuma na zinki ni muhimu sana katika mwili wa binadamu
Alibainisha maharage haya
yanamadini ya chuma ambayo yanasaidia kuongeza chembechembe nyekundu za damu ambazo ni muhimu sana kwenye kusafirisha hewa ya
oksijeni kwa ajili ya uhai hivyo ni
muhimu jamii ikiajijengea tabia ya kutumia maharage haya
Mtafiti huyo alienda mbali na
kusema kuwa Tanzania iliweza kupitisha
aina mbili za mbegu bora zenye madini
ya chuma na zinki kwa wingi ambazo alizitaja mbegu hizo kuwa ni Selian14 pamoja
na Selian 15 .
Alibainisha kuwa Takwimu za
afya na viashiria vya malaria iliyofanywa mwaka
2015-2016inaonyesha kuwa upungufu wa samu kwa watoto wenye umri wa kati
ya miezi sita -59ni kwa asilimia 58 ambapo asilimia 26wanaupungufu wa damu
wakawaida na asilimia 30 wanaupungufu wa damu wa kati huku asilimia mbili
wanaupungufu wa damu wa juu.
Alifafanua kuwa asilimia 45
ya wanawake wa Tannzania walio katika umri wa uzazi kuanzia miaka 15 hadi miaka
49 baadhi yao wanakabiliwa na tatizo hilo la upungufu wa damu ambapo kati yao
asilimia 33wanaupungufu wa damu wa kawaida na asilimi 11 wanaupungufu wa damu
wa kati na asilimia moja wanaupungufu wa damu kwa kiwango kikubwa zaidi ,alibainisha
kuwa asilimia 70 ya vifo
vinavyosababishwa na upungufu wa damu hutokea katika nchi za afrika
Aidha mathara mengine
yanayosababishwa na upungufu wa madini ya chuma ni pamoja na mwili kuchoka mara
mawazo ,hivyo kutokana na takwimu hizi
na tatizo hio kubwa la kiafya na kilishe waliona jamii inaitaji ufumbuzi
wa lishe kwa haraka hivyo wakaona
nivyema watafute ufumbuzi huo na ndio wakaja na aina hizi mbili za maharage
Sifa ya maharage ya seliani
14 yanakiwango cha madini ya zinki 26.38kwa 41.65ppm nakiwango cha madini ya
chuma 75.17-8535ppm muda wa kuyapika ni kuanzia dakika 19-40 pia yanaladha tamu
na unaweza kupika kwa mchanganyiko wowote na hayaaribiki ladha
Sifa ya maharage ya
selian15 kiwango chake cha madini ya
chuma ni 74.22-8135ppm yanakiwango cha madini ya zinki 27.38-42.55ppm yanapikwa
kwa muda wa dakika 19-40.
Kutokana na sifa za maharage
haya ni vyema wananchi wakajitaidi kuyatumia katika milo yao hususa ni wale
wanaotarajiwa kubeba ujauzito na hata
kwa watoto ambao wanatatizo la kupungukiwa damu.
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia