BREAKING NEWS

Saturday, April 2, 2022

WAKULIMA WADOGO WA MIWA KUONDOKANA NA TATIZO LA KUKOSA MASOKO

 

Mhandisi Profesa Fredrick Kahimba akiongea na waandishi wa habari walipokuwa katika ziara ya mafunzo ya kuandika habari za sayansi na teknnolojia yalioandaliwa na Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Sayansi Teknolojia na Ubunifu (COSTECH) (habari na picha na Woinde Shizza ).

Wakulima wadogo na binafsi wa miwa nchini wanatarajia kuondokana   na changamoto ya kukosa masoko ya bidhaa zao baada ya taasisi ya Uhandisi na Usanifu Mitambo nchini (Temdo) kutengeneza mitambo midogo yenye uwezo wa kuzalisha tani moja hadi 10 za sukari kwa saa moja.

Akizungumza  jijini Arusha katika mafunzo kwa Waandishi wa Habari kutoka Kanda ya Kaskazini na yaliyoratibiwa na tume ya taifa ya Sayansi Teknolojia na Ubunifuni (COSTECH), mkurugenzi mkuu wa TEMDO Mhandisi Fredrick Kahimba alisema kuwa kukamilika kwa mashine hii kutamrahisishia sana mkulima kuzalisha sukari kiurahisi

Alisema  kuwa mara nyingi viwanda huwa vinavuna kwanza miwa yao kisha uangalia iwapo wanahitaji miwa zaidi kutoka kwa wakulima binafsi ambayo mara nyingi ni sehemu ndogo tu hivyo wakulima wengi wamekua wakikosa soko.

“Katika kipindi cha mwaka 2021/2022 tutakua tumetengeneza mashine mbili za mfano ambazo tutazipeleka kwa wakulima ambao watatupa mapendekezo ya mwisho ambayo tutayazingatia kwenye utengenezaji wa mashine na  zaidi pia tunatarajia hadi kufikia mwezi april tutakuwa tumemaliza mashine moja ,” amesema Profesa Kahimba

Amesema utengenezaji wa mashine hizo utakua mkombozi kwa wakulima wa miwa nchini ambao wataondokana na utegemezi wa kuuza miwa yao viwandani na kuanza kuchakata miwa yao kwaajili ya kuzalisha sukari ambayo kwa nyakati tofauti nchi imekua ikipata upungufu.

Akizungumza  jijini Arusha katika mafunzo kwa Waandishi wa Habari kutoka Kanda ya Kaskazini na yaliyoratibiwa na tume ya taifa ya Sayansi Teknolojia na Ubunifuni (COSTECH), Mkuu wa Kitengo cha mawasiliano na masoko kutoka TEMDO, Dk. Sigisbert Mmasi alisema kuwa  TEMDO kwa zaidi ya miaka 30 wametengeneza mashine za aina mbalimbali za kilimo, viwandani pamoja na kutoa elimu kwa wahandisi na mafundi uchundo nchini.

 

 

Share this:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

 
Back To Top
Copyright © 2014 MOUNT KILI NEWS. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates