Ticker

6/recent/ticker-posts

HATIMAYE CHUO CHA ATC WANATARAJIA KURUSHA HELKOPTA ANGANI


Na Woinde Shizza,Arusha
CHUO cha ufundi Arusha, ATC, kinatarajiwa kukamilisha matengenezo ya Helkopita na kuirusha angani mapema mwaka 2018 na kuwa ni chuo cha kwanza nchini kurusha Helkopita iliyotengenezwa na Mhandisi mzawa.

Hayo yameelezwa jana na Mhandisi wa ufundi aliyebuni na  anayetengeneza Helkopita hiyo, Abdi Mjema, kwenye hafla ya chuo hicho kukabidhiwa maabara ya maji mwendo ambayo imejengwa na serikali ya Japan,kupitia shirika lake la misaada la JICA, chuoni hapo.

Mhandisi Mjema ,amemwambia katibu mkuu wa wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia, Maimuna Tarishi, kuwa matengenezo ya Helkopita hiyo ambayo ameibuni yamefikia asilimia 40, na anafanya matengenezo hayo kwa kuwasiliana na mamlaka ya viwanja vya ndege kwa kila hatua anayofikia.

Amesema hatua ya majaribio ya kuirusha Helkopita hiyo ambayo inatengenezwa kwa malighafi za nchini anatarajia kuyafanya wiki tatu zijazo  mara baada ya kukamilisha hatua iliyopo sasa ambapo ni 40% ya matengenezo na ambapo utengenezaji wa Helkopita hiyo anatarajia kuukamilisha mwishoni mwa mwaka 2017 .

Mjema, ambae ni mtaalamu wa mitambo aliyebobea  pia mhadhiri wa chuo hicho cha serikali cha ufundi,amesema wazo hilo la kubuni Helkopita hiyo aliibua kutokana na changamoto za usafiri zilizopo nyumbani kwao wilayani Mwanga, ambayo eneo kubwa ni milima na wakati wa masika maeneo mengi huwa hayafikiki.


Post a Comment

0 Comments