Ticker

6/recent/ticker-posts

RAIS MAGUFULI AOBWA KUINGILIA MMGOGORO WA HALMASHAURI NA WANANCHI

Na Woinde Shizza,Arusha
WANANCHI 43 wakazi wa eneo la Mianzini, Timbulo wilayani Arumeru mkoani Arusha,wamemwomba Rais John Pombe Magufuli kuingilia kati Mgogoro dhidi yao na  Halmashauri ya Arusha kufuatia Halmashauri hiyo kukaidi hukumu ya mahakama iliyo elekeza wananchi hao kulipwa fidia katika upanuzi wa barabara yenye urefu wa kilometa 8.



Wakizungumza na vyombo vya habari jana moja ya wananchi hao, Fanuel Lamai na wenzake sita walio fungua kesi , kwa niaba ya wananchi hao alisema kuwa mwaka 2013 walifungua kesi ya ardhi namba 18 katika mahakama kuu mkoani Arusha dhidi ya halmashauri ya Arusha wakipinga hatua ya kubomolewa nyumba zao bila kulipwa fidia katika mradi wa upanuzi wa barabara ya Mianzini Timbulo  unaotekelezwa na halmashauri ya Arusha.

 .

Alisema kuwa bara bara hiyo ambapo hapo awali upanuzi wake ulitakiwa kuwa mita 10 kwa 10 wananchi hao walipinga na kueleza mahakama kuwa bara bara hiyo haikuwepo wakati wananchi hao wana anzisha makazi kwani kipindi hicho eneo hilo lilikuwa ni njia ya mapito ya mifugo.



Katika hukumu ya kesi hiyo iliyotolewa na Jaji Fatma Massengi wa mahakama kuu alielekeza  upanuzi wa barabara hiyo ufanyike mita 4 kwa 4 badalaya ya mita 10 kwa 10 na ikasema ipo haja kwa halmashauri na wananchi hao kukaa na kuridhiana iwapo itaongeza kiwango cha upanuzi hukumu ikielekeza kuwa wananchi hao wanapaswa kuendelea kuishi kwenye ardhi yao .



Wananchi hao wamesikitishwa na hatua ya halmashauri kuanza upanuzi wa barabra kwa kubomoa nyumba zao zaidi ya 30 zilizofunjwa hadi sasa bila kujua iwapo watafidiwa kama mahakama hilivyo elekeza.



Wananchi hao wakiwemo wazee na wajane wamemwomba Rais Magufuli kuingilia mgogoro wao kwa kuiamuru halmashauri isitishe zoezi la kuvunja nyumba zao hadi hapo watakapo patiwa fidia wanazo dai zinazofikia kiasi cha shilingi bilioni 3.

Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha Lembris Noha alisema kuwa halmasahuri hiyo aitalipa fidia kwa wananchi hao  na wanasimamia sheria ya ardhi ya mwaka 1932 inayo elekeza kuwa upanuzi wa bara bara mita 10 kwa 10 auna fidia na kuwataka wananchi hao kusoma vizuri hiyo hukumu na kuelewa na wasikurupuke kuwadanganya wenzao ambao wameelewa na kuanza kubomoa wenyewe nyumbza zao .


Post a Comment

0 Comments