Ticker

6/recent/ticker-posts

"TUMEANZA KUBAINI MAABARA FEKI AMBAZO HAZIJASAJILIWA NA ZINATOA HUDUMA KINYUME NA UTARATIBU "DKT SIMONI CHACHA

Image result for nembo ya jiji  la arusha
 
Mganga mkuu wa wilaya ya Arusha mjini Dokta Simoni Chacha kwa kushirikiana timu yake ya mkoa imeanza kufanya operesheni maalum ya kukagua maabara zote binafsi ili kubaini zile ambazo hazijasajiliwa na zilizokosa sifa ya kutoa huduma katika jiji la Arusha.
Akizungumza na waandishi  Dokta Chacha amesema kuwa zoezi hilo limeanzia katika eneo la matejo kata ya Ngarenaro ambapo wamekuta maabara ijulikanayo kwa jina la Sonogesha ambayo inatibu wagonjwa kinyume cha taratibu.
Akizungumzia sifa za maabara zinazotakiwa Dokta Chacha amesema kuwa  lazima ziwe na watumishi wa kutosha,cheti za usajili,vyumba vya kutosha kwa ajili ya huduma na maeneo ya kutosha huku akisema zoezi hilo ni endelevu na hawatawaonea mtu huruma.

Hata hivyo maabara ambazo zimetembelewa zimegundulika  kuwepo kwa mapungufu kama vibali kuisha muda wake na kutoa huduma kinyume na taratibu utoaji wa dawa,kupima vipimo ambavyo hawakuruhusiwa na kama vile Typhod na kukosa watumishi wenye sifa.
 
Vile vile maabara zilizopewa maelekezo  na kupewa onyo ili waboreshe huduma ni maabara ya TRUST health Laboratory service,Amani labaratory ,Arusha Jonior ,Global Medicare, na morden klinic 
Kwa upande wa wananchi wa jiji la Arusha wamepongeza zoezi hilo ambalo wameanza huku wakibainisha kuwa maabara nyingi zimekuwa zikitoza fedha nyingi kwa kutoa huduma ambazo hazilingani na fedha wanayotoa.

Post a Comment

0 Comments