MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO AKANUSHA KASHFA YA UPORAJI WA ARDHI YA WANANCHI


Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Leonidas Gama akizungumza na wanahabari (hawako pichani) juu ya tuhuma zilizoibuliwa bungeni dhidi yake.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama akiwa na mkuu wa wilaya ya Moshi,Novatus Makunga katika mkutano huo na wanahabari.

Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali ya habari mkoani Kilimanjaro.



SIKU moja baada ya kambi rasmi ya Upinzani Bungeni kumlipua mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Leonidas Gama kwa madai ya kufanya udalali na ufisadi katika uporaji wa ardhi ya wananchi ,mkuu huyo amejitokeza
mbele ya wanahabari na kukanusha tuhuma hizo.

Katika utetezi wake Gama alirejea kauli yake aliyoitoa miaka sita iliyopita ya kuwa yeye ni msafi huku akiitupia mzigo halmashauri ya wilaya ya Rombo tuhuma za kiasi cha sh Mil 500 zilizotajwa kutolewa wawekezaji wa Kichina kama fidia kwa wananchi katika ardhi
kilipojengwa kiwanda cha kutengeneza Saruji.

Alisema tuhuma zilizotolewa Bungeni dhidi yake si za kweli na kwamba ni za kisiasa huku akitaja sababu ya kuibuliwa kwa tuhuma hizo kuwa ni kutokana na juhudi zake za kupambana na Pombe haramu katika wilaya ya Rombo pamoja na Urejeshwaji wa wafanyabiashara katika soko la kati la mjini Moshi.

“Nataka niwaambie hii ni siasa,zipo issue nyingi zilizochangia kuibuka kwa haya mambo ,lakini nawaambieni mbili tu,Issue ya kwanza Pombe Rombo,na msimamo wangu juu ya Pombe Rombo ndio imeza hii,la pili ni
soko la Moshi mjini,watu wana agenda zao kwenye soko hilo ,wananchi wamerudi pale ,imewaumiza watu.”alisema Gama.

“Watu walitaka Pombe ya Gongo iharalishwe,mimi nimesema hadharani anayetaka pombe ya Gongo ihararishwe si mwenzetu mu mshughulikie kwa maana si mwenzetu sasa hili limeleta nongwa”aliongeza Gama.

Akitoa ufafanuzi juu ya tuhuma hizo ,Gama amekiri mtoto wake aliyetajwa kwa jina la Mayunga Leonidas Gama kuhusika katika uanzishaji wa kiwanda hicho huku akihakikisha kiwanda hicho kinajengwa katika mkoa wa Kilimanjaro badala ya Bagamoyo kama walivyo pendelea
wawekezaji hao.

“Kiwanda cha saruji kinachojengwa pale Rombo, nilikuwa na uwezo wa kukipeleka popote ninapotaka mimi, lakini mimi binafsi ndiye niliyefanya juhudi kiwanda kile kijengwe Kilimanjaro, mimi binafsi na wala sio mtu mwengine, nimefanya juhudi hizo kwa lengo la kuongeza
ajira kwa wananchi na kuinua uchumi wa mkoa huu”, alisema Gama .

“Historia ya Kiwanda hiki iko wazi, na  nililipeleka hadi kwenye kikao cha ushauri wa mkoa (RCC),nanaomba nieleweke kwamba, ni juhudi zangu na za mtoto wangu, nilitamka kwenye kikao kile na wala sikuficha, mtoto wangu ambaye ametajwa yeye ana rafiki yake wa kichina, wala si
kweli kwamba hii kampuni mimi nimekwenda kuichukua China kwa gharama za serikali” aliongeza Gama.

Alisema katika kikao hicho (RCC), Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini, Mbunge wa Vunjo, Dkt. Augustino Mrema na Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo, walishiriki katika kikao hicho na kwamba baada ya mvutano ndipo makubaliano yakawa kiwanda kijengwe wilaya ya Rombo .

“Toka siku ile mimi kama mkuu wa mkoa nikakabidhi madaraka wilaya yaRombo,kwa hiyo shughuli zote za ujenzi ,shughli zote za kutafuta viwanja ziifanywa na halmashauri ya wilaya ya Rombo na sio Gama”alisema Gama.

Alisema waliolipa fidia na kununua viwanja ni halmashauri ya wilaya na hata eneo

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia