Ticker

6/recent/ticker-posts

KAMPUNI YA TBL YANYAKUWA UBIGWA WA JUMLA WA MWAJIRI BORA

 Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya TBL group wakiwa katika picha ya  pamoja muda mfupi baada ya kampuni yao kuibuka mshindi wa jumla wa tuzo ya mwajiri bora inayotolewa na Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE) katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Mlimani City mwishoni mwa wiki.
 Waziri Mkuu Mh.Kassim Majaliwa (kulia) akimkabidhi  kombe la tuzo ya mwajiri bora kwa Mkurugenzi wa Raslimali Watu wa TBL Group,David Magese (Kushoto) katika hafla iliyoandaliwa na Chama Cha Waajiri Tanzania na kufanyika katika ukumbi wa Mlimani City mwishoni mwa wiki ambapo TBL iliibuka kwa mshindi wa tuzo hiyo kwa mwaka 2015,(katikati) ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck sadiki.
Waziri Mkuu Mh.Kassim Majaliwa ( wa nne kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa serikali,viongozi wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) na wafanyakazi wa kampuni ya TBL Group muda mfupi baada ya kuitunukia kampuni hiyo tuzo ya mwajiri bora kwa mwaka huu katika hafla iliyoandaliwa na Chama Cha Waajiri Tanzania na kufanyika katika ukumbi wa Mlimani City mwishoni mwa wiki.

Post a Comment

0 Comments