Ticker

6/recent/ticker-posts

SJHAGWE ZA COKE STUDIO ZAZIDII KULETA BURUDANI NDANI YA JAMII

 Mwanamuziki Ali Kiba na Victoria Kimani wakiwa katika onyesho la Coke Studio
 Wanafunzi kuanzia shule za msingi nchini hadi vyuo vikuu wameshiriki kuonyesha vipaji vyao katika msimu huu wa Coke Studio  kama wanavyoonekana  katika moja ya tamasha la Coke Studio
Wasanii wa muziki wakitoa burudani katika moja ya tamasha la Coke Studio mkoani Mwanza
Mwanamuziki Fid Q akitoa burudani katika moja ya tamasha  la Coke Studio

-Wanafunzi na vijana mitaani waendelea kupata burudani
Onyesho la Coke Studio msimu wa tatu linaloendelea linazidi kuleta burudani na furaha kwenye makundi mbalimbali ya jamii na kuacha gumzo kwa wengi nchini.
Vijana wengi wameeleza kuwa pamoja na kuburudika na  maonyesho ya kolabo za wanamuziki machachari yanayoonyeshwa kupitia luninga ya Clouds kila siku ya Jumamosi na kwenye redio ya Clouds bado wamekuwa wakipata burudani kutoka matamasha shirikishi yanayoendelea kwenye mikoa mbalimbali na kushirikisha watu kutoka makundi mbalimbali ya jamii.
Wanafunzi kutoka shule mbalimbali walipohojiwa juu ya onyesho hili walisema kuwa linaleta raha na burudani huku likiibua vipaji na kuwakutanisha vijana na watu wanaojiamini ambao wamefanikiwa kwenye mambo wanayoyafanya.
“Coke Studio ni zaidi ya burudani kwa kuwa pia inatuwezesha vijana kuonyesha vipaji wakati huo huo kukutana na watu ambao wanajiamini ambao wamefanikiwa katika mambo yao”.Alisema Willy Chale Mwanafunzi wa Sekondari ya Mwanza.
Miriam Chande mwanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa fedha alisema analipenda onyesho la Coke Studio kwa kuwa linatoa burudani ya aina yake ya muziki ambayo imewalenga vijana na inawawezesha kupata jumbe za kuwahamasisha kusonga mbele kimaendeleo.
Kassim Juma,mwendesha bodaboda na mwanamuziki wa kujitegemea amesema kuwa yeye na wenzake wanapenda onyesho la Coke Studio kwa kuwa ni la viwango na limelenga kutoka burudani kwa  makundi mbalimbali kupitia kuangalia kolabo za wanamuziki na matamasha ya muziki na burudani yanayoendelea sehemu mbalimbali nchini.
Msimu wa Coke Studio mwaka huu umeshirikisha wanamuziki mbalimbali kutoka Tanzania na nchi za nje
Wanamuziki hao ni Fid Q ambaye amefanya kolabo (mash-up) na Maurice Kirya na Vanessa Mdee ambaye amefanya kolabo (mash-up) na mwanamuziki 2face kutoka Nigeria , Ali Kiba na  Victoria Kimani na Ben Paul na wangechi.
Msimu huu wa Coke Studio umeambatana na kampeni mpya yenye jina la ‘Sababu Bilioni za Kuamini’, na hivyo kujumuisha vijana mbalimbali ambao wanaamini katika kufikia malengo yao bila ya kujali changamoto zinazowakabili.
Lengo kuu la Coke Studio Afrika ni kuwakutanisha kwa pamoja wasanii wenye mbalimbali wa Afrika na kuimba nyimbo ambazo zina vionjo tofauti hivyo kuongeza msisimuko. Lakini vilevile kutoa fursa kwa wasanii wachanga  kushirikiana na wakubwa ili kuwapa changamoto ya kuongeza ujuzi katika kazi zao na kuzidi kukuza vipaji vyao
  

Post a Comment

0 Comments