Ticker

6/recent/ticker-posts

HALMASHAURI ZA MONDULI ,LONGIDO NA ARUMERU WATAKIWA KUONGEZA KASI UPATIKANAJI WA FEDHA ZA LISHE

 Na Woinde Shizza , ARUSHA


Halmashauri za wilaya ya Monduli,longido na Arumeru zimetakiwa kufanya jitihada zaidi katika uchangiaji wa fedha zinazotengwa na halmashauri kwa ajili ya lishe ili kupunguza tatizo  ya lishe duni kwa Watoto wenye umri chini ya miaka mitano.

 Hayo ya mebainishwa na kaimu mwenyekiti wa kamati ya lishe mkoa wa Arusha Mosses Mabula alipokuwa akiongea katika kikao cha kujadili mwenendo wa hali ya lishe ndani ya mkoa wa Arusha ambapo pamoja na mambo mengine ambapo walitakiwa  kuhakikisha halmashauri zote zinachangia fedha kwa ajili ya lishe 

Aidha alitoa msisitizo kwa kwa zile halimashauri ambazo hajifikia lengo kufanya hivyo mara mojo ili kuweza kufikia malengo yaliyokusudiwa.


Alitaja mikakati ya kubadilisha hali ya lishe katika mkoa wa Arusha imewekwa  ni kuhamasisha halmashauri ambazo hazijatekeleza mpango huo wa kuchangia na kutumia fedha za lishe kufanya hivyo ili mkoa uweze  kurudi katika alama ya kijani.


 
Kwa upande wake afisa lishe mkoa wa Arusha Rose Mauya  alisisitiza ushirikishwaji wa wananchi katika mpango huo wa lishe ni jambo linalopewa kipaumbele ili kutoa elimu ya uelewa katika suala hilo

Post a Comment

0 Comments