SHIBUDA ANG'OLEWA UONGOZI ADA-TADEA

 






Na Woinde Shizza,ARUSHA

Imeelezwa kuwa kuonyesha mwanga ni dira ya demokrasia kwa Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Samia Suluhu kumepelekea  baaadhi ya migogoro  kuibuka ndani ya  vyama mbalimbali vya upinzani .

Akiongea na waandishi wa habari katibu wa itikadi na uwenezi  taifa wa chama cha ADA-TADEA  Zubery Mwinyi alisema kuwa ndani ya vyama vya upinzani kwa sasa kila mtu  anajitokeleza kutaka kupata nafasi  kwa kuwa kipindi  hichi cha uongozi wa Rais  Samia ni nafasi pekee ya kwenda kufanya siasa ambazo niza kweli na za utafiti

“kutokana na hayo ya kutaka nafasi ndani ya vyama ndio maana vyama vingi vinakuwa na migogoro na h ii ni ndio sababu  wapo ya kuleta migogoro  ndani ya vyama lakini tunasema kwamba Rais samia ametuonyesha  dira  kubwa katika siasa  na ni mtu ambae anania ya kweli  na nimkweli na ndio kitu ambacho kilikuwa kina subiriwa sana nawapinzani ndani ya Tanzania natuseme  tu kwa sasa watanzania tumepata kiongozi ambaye ni mkweli na muwazi na tunaamini ataifikisha nchi yetu mbali”alibainisha Zuberi

Wakati huo huo  katibu mwenezi  huyo alisema kuwa chama hicho chama  cha siasa cha ADA –TADEA  kimepata viongozi wapya huku aliekuwa  katibu mkuu John Shibuda akiwa amemwagwa katika   uchaguzi uliofanyika June  28  katika ukumbi wa  lego uliopo jijini Dar es salaam .

Alisema kuwa kwa upande wanafasi ya  mwenyekiti  imechukuliwa na  yule yule Juma Ally Khatibu  huku makamu wake kutoka Tanzania bara ni Zaituni  Hokohoko ,makamu mwenyekiti  Zanzibar ni Hassan Kijigoo,huku katibu mkuu  akiwa Salehe Mhomamed Msumari ,naibu katibu kuu bara ni Georia’s Busungu  ,Naibu katibu mkuu Zanzibar  Hamis Mambo, nafasi ya katibu Mwenezi taifa Zuberi Mwinyi ,naibu katibu mwenezi  Zanzibar Halima  Abdaallah  huku naibu  katibu mwenezi  bara  akiwa Ireen Anatory.

Alibainisha  viongozi hawa wapya waliochaguliwa ni vijana hivyo  wamejipanga kukipambania chama chao ili kiwe chama cha kwanza cha upinzani kinachoongoza hapa  nchini .

Aidha alibainisha baadhi ya mikakati waliokuwa nao kama chama ni kuakikisha  kila mkoa chama kinatambulika na  wananchi na kinasaidia kuboresha maendeleo ya wananchi

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

Previous Post Next Post