KAMATI YA UONGOZI NA WATAALAM JUU YA MGOGORO WA NGORONGORO IMESEMA INAAMINI SERIKALI ITATOA MATOKEO CHANYA

 

Picha na maktaba

Na Woinde Shizza,ARUSHA

Kamati ya viongozi na wataalamu juu ya mgogoro wa Ardhi ya Tarafa ya Ngorongoro, Sale na Loliondo waliosilisha taarifa ya kukusanya mapendekezo kwa wananchi nakuwasilisha katika Ofisi ya Waziri mkuu wa Jamuhuri ya muungano imesema kuwa inaamini serikali itatoa matokeo chanya kwa ajili ya ustawi wa wananchi wa Ngorongorona utaleta suluhu katika utatuzi wa migogoro ya ardhi katika eneo lenye kilometa za mraba 1500 bila kuathiri pande zote mbili


Hayo yameelezwa na  Mwenyekiti wa kamati hiyo,Metui Sheudo wakati akiongea na waandishi wa habari mkoani Arusha  ambapo alisema  mchakato huo wa mapendekezo ya wananchi umedumu kwa muda wa miezi mitatu ikiwa lengo ni kuwafikia wananchi katika kutoa mapendekezo yao.




Alisema kuwa wanatumatumaini  kuwa mapendekezo hayo yatatolewa   matokeo chanya kwa ajili ya ustawi wa wananchi wa Ngorongoro na italeta suluhu katika utatuzi wa migogoro ya ardhi katika eneo lenye kilometa za mraba 1500 bila kuathiri pande zote mbili


Metui alisema hatua hiyo ilifuata baada ya mchakato wa kuwashirikisha wananchi na makundi mbalimbali katika jamii kuwa hafifu katika kutatua mgogoro huo.


Kwa upande wake diwani wa kata ya Nainoka noka,Edward Maura alisema wanaishukuru serikali kupitia ofisi ya waziri mkuu kwa kutoa fursa kwa wananchi wa wilaya ya Ngorongoro kuunda kamati na kuandika mapendekezo ya jamii juu ya mwenendo wa changamoto zilizopo wilayani hapo.






Vilevile alisema japo matatizo yanawapelekewa kuhamishwa ni pamoja na zilezinazoelezwa ni wingi wa mifugo pamoja na ongezeko la watu kwa mujibu wa serikali pia wao kama Wananchi wameongeza matatizo mengine ikiwemo uwepo wa magugu vamizi






Alibainisha  kupitia kamati iliyokuwa na wajumbe wa pande zote katika jamii wameikamilisha kazi kutokana na ushirikiano baina ya wananchi na wanakamati hali iliyoleta tija katika kuandika taarifa hiyo waliyoiwasilisha serikalini






Aidha  walimshukuru waziri mkuu kwa kupokea taarifa hiyo japo kuwa tayari kulikuwa na maneno ya chini chini kuwa hata pokea  na kuhiadi serikali kupitia Mbunge wa Ngorongoro kurudi kwa ajili ya majadiliano hivyo wanategemea taarifa hiyo kutoa mateokeo chanya.

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

Previous Post Next Post