TEMDO YATAKIWA KUPELEKA KIWANDA CHA KUCHAKATA SUKARI KILOMBERO KABLA YA MWEZI DECEMBER


meneja wa karakana  ya Taasisi ya uhandisi na usanifu mitambo Tanzania (TEMDO) Nicas Bernard akimuonyesha 
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji,  Dkt.Ashatu Kijaji pamoja na ujumbe wake Moja ya kifaa Cha mashine ya kuchakata miwa kinachotengenezwa na  tahasisi hiyo juzi wakati waziri huyo alipotembelea kiwanda kicho kuona namna wanavyofanya


 Na Woinde Shizza,ARUSHA

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji,  Dkt.Ashatu Kijaji ameiagiza Taasisi ya uhandisi na usanifu mitambo Tanzania  (TEMDO) kabla ya mwezi December wawe wamepeleka mitambo wa kuzalisha ,na kuchakata  sukari   kwa wananchi wanaoishi katika wilayani Kilombero ili kuweza kupunguza tatizo la upotevu wa miwa mingi inayolimwa na wananchi wa  wilaya hiyo.


Aliyasema hayo wakati akiongea na wafanyakazi wa taasisi hiyo alipofanya ziara ya kuitembelea na kuona namna wanavyofanya kazi  ambapo aliipongeza taasisi jinsi wanavyofanya kazi na kuwasihi waendelee kufanya kazi Kwa nguvu na Kwa Kasi zaidi


Alibainisha Wananchi wa sehemu za Kilombero ,mtibwa na sehemu zingine zinazolima zao la miwa ,mazao yao yamekuwa yakiharibikia sokoni kutokana na kukosa sehemu za kupeleka hivyo ni vyema wao kama Temdo ambao teyari wameshabuni na kutengeneza mtambo wa kutengeneza sukari wakaanza kupeleka mitambo hiyo katika sehemu izo Ili kuweza kuwapunguzia Wananchi adha ya kukosa sehemu ya kuuzia miwa yao.


"Ninajua sehemu ninyingi zinazolima miwa zinauhitaji ila nataka niwape kazi temdo adi ukifika mwezi December muwe mmeshawapelekea Wananchi wa mtibwa huo mtambo  na baada ya Kilombero mpelekee na kwingine kama mtibwa na hata hapo Kilimanjaro  kama Wananchi wanauitaji na icho kiwanda kinashidwa kuchukuwa na miwa yote ya Wananchi  basi mnapeleka mashine ambayo itawasaidia Wananchi na uzuri wa mtambo huu mmesema  unaweza kuwekwa hata nyumbani hauchukui sehemu kubwa  naniwaambie tu Serikali inaela ya kutosha nyie kazi yenu ni kufanya kazi tu tena kwa kasi lazima tuwe na haraka maana tumechelewa  tukimbie zaidi kwenda kwenye uzalishaji"alibainisha Kijaji


Alisema bainisha kuwa katika kipindi wizara hiyo ilivyokuwa ikiwakilisha bajeti yao bungeni ,wawakilishi  wa wananchi bungeni walilalamika sana kuhusiana  na miwa ya Wananchi kutupwa kutokana  na viwanda vilivyopo kushidwa kuchakata miwa  yao yote  hivyo ni lazima tuwaonyeshe watanzania tupo na tunafanya kazi Kwa kuanza kupeleka mtambo huo Kilombero

"Miwa inatupwa Kwa nini kwa sababu viwanda haviwezi kuchakata miwa yote maana hii tunawazibiti wananchi wasilime miwa kwanini Kwa sababu hamna pakupeleka Sasa sisi Kama serikali   tunakwenda kujibu matatizo ya Wananchi Kwa kuchukuwa ichi kiwandakili chotengenezwa na   temdo cha milioni 500  tuwapelekee Wananchi wa pale Kilombero ,tunawawezesha vijana watanzania wamesoma waweze kuendesha waweze kusaga kuchakata miwa ya Wananchi na tutoe  sukari ili tatizo la sukari liweze kuisha kabisa hapa nchini, wenzetu wa nje ya nchi mfano uganda ambapo tunaagiza sukari wameweza kwakuwa wameweza kwakuwa wamewezesha hivi viwanda vidogo vidogo  na sisi Temdo , CAMARTEC ndio kazi yetu "alisema Kijaji

Aliwapongeza TEMDO  Kwa kuanza kutengeneza vifaa tiba na kuwaahidi kuwa katika kutatua tatizo lao la kukosa wateja wa vitanda vya nahospitali atahakikisha analimaliza Kwa kuwatafutia wateja na kuwasemea nakuwatangaza katika kila sehemu ambayo atakuwa anaenda.

Kwa upande wake mkurugenzi  wa tasisi hiyo Muhandisi Fredrick   Kahimba alisema kuwa wamepokea maelekezo hayo na wapo tayari kuyafanyia kazi Kwa Kasi kama vile serikali ilivyoagiza 


 Kahimba alisema kuwa katika taasisi hiyo wamekuwa wakipata  tatizo la  kupata wateja wa vitanda wanavyovitengeneza   Kwa ajili ya hospital  kwani wametengeneza vitanda lakini tatizo kubwa walilonalo ni sehemu za kuviuzia  ambapo alifafanua kuwa vitanda hivyo pamoja na vifaa tiba vingine walivyotengeneza vimeshapimwa na Kupata idhibati kutoka taasisi husika ikiwemo TMDA.

Aidha pia alisema kuwa kutengeneza vifaa tiba hivyo vimesaidia kuongeza ajira za ndani na kurahisha upatikanaji wa bidhaa kirahisi na kwa bei nafuu huku akifafanua kuwa kwa sasa TEMDO inavifaa tiba zaidi ya kumi na tano (15) ambapo pia alizisihi taasisi za serikali na binafsi kujitokeza Kwa wingi kwenda kuagiza vifaa tiba hivyo.

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

Previous Post Next Post