Ticker

6/recent/ticker-posts

NEC - YAFUNGUKA YASEMA MAANDALIZI YA UCHAGUZI YAKO SAFI


  Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Damian Lubuva akiteta jambo na Kamishna wa Tume hiyo, Jaji mstaafu Vincent Msena


TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imesema maandalizi ya Uchaguzi Mkuu ujao, yamekamilika na kuwataka wananchi kufika katika vituo vya kupigia kura siku nne kabla ya uchaguzi ili kuhakiki majina yao.

Mkurugenzi wa Uchaguzi kutoka NEC, Bw. Ramadhan Kailima, aliyasema hayo jana wakati akizungumza na Wahariri wa vyombo vya habari na kufafanua kuwa, wameandaa vituo 72,000 nchini kote ambacho kila kimoja kitakuwa na uwezo wa kuhudumia watu 450.

Alisema uandikishaji wapigakura kwenye Daftali la Kudumu umefanyika kikamilifu kwa kutumia mfumo mpya wa BVR ambapo hadi sasa, watu milioni  23 wameandikishwa na idadi kamili itatolewa wiki ijayo.

"Siku ya kupigakura vituo vitakuwa wazi kuanzia saa moja asubuhi na kufungwa saa 12 jioni...wapigakura hawaruhusiwi kubaki kwenye vituobaada ya kupigakura ili kuondoa malumbano  yanayoweza kuleta uvunjifu wa amani," alisema Bw. Kailima.

Aliongeza kuwa, majimbo ya uchaguzi yako 264, kata 3,957 ambazozitashiriki uchaguzi na NEC ndiyo yenye dhamana ya kutangaza matokeobaada ya kubandikwa kwenye vituo vya kupigia kura na kuhakikiwa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Damian Lubuva, alisema katika baadhi ya majimbo na kata, uchaguzi umesitishwa kutokana na vifo vya wagombea wabunge, madiwani. 

Majimbo hayo ni Lushoto (Tanga), Ulanga Mashariki (Morogoro) na udiwani Kata za Bomang'ombe, Bukene, Msingi Mkalama, Muleba na Uyola ambayo uteuzi wa wagombea wake utafanyika Oktoba 12, kampeni zitaanza Oktoba 13 hadi Novemba 18, mwaka huu na kura zitapigwa Novemba 22, mwaka huu," alisema.

Post a Comment

0 Comments