BREAKING NEWS

Thursday, January 14, 2016

Studio ya Music ya 'The Industry' Inayoongozwa na Producer Nahreel Yamtangaza Rasmi Msanii Mpya wa Kike Aliyejiunga Nao


THE INDUSTRY MUSIC LABEL

TAARIFA KWA UMMA

UTAMBULISHO WA MWANAMUZIKI MPYA WA STUDIO YA MUZIKI YA “THE INDUSTRY”


Uongozi wa Studio ya Muziki ya The Industry iliyoko chini ya Wanamuziki Producer Nahreel na Aika Marealle unapenda kuchukua Nafasi hii kuwatangazia Umma Kuwa kuanzia Tarehe 14 January 2016 Wamemuingiza Msanii mpya wa Kike aitwaye Rosa Ree, Rose Ree ni muimbaji wa Muziki aina ya Rap ambae kazi zake zitaanza kusikika/Kuonekana siku si nyingi kuanzia sasa katika Redio Mbali mbali na TV Stations za Tanzania na nje ya nchi.

Kama wasikilizaji na watazamani tunaomba Kumuunga mkono Msanii huyu mpya Kwani tuna uhakika hatawaangusha katika kuwaletea burudani Katika Masikio na macho yenu pindi kazi zake zitakapoanza kutolewa hivi karibuni.

The Industry ni studio na kampuni ya muziki ambayo ipo chini ya kundi la music lenye Mafanikio makubwa la Navy Kenzo ikisimamiwa na Producer Nahreel na msaidizi wake Aika Marealle

Wasanii Baadhi Waliokwisha fanya kazi na Studio ya The Industry mpaka sasa toka kuanzishwa kwake hivi karibuni ni Diamond Platnumz na wimbo wake wa Nana, Nikki wa Pili na wimbo wa Baba Swalehe, Joh Makini na nyimbo zake kama Don’t Bother na nusu nusu.

Imetolewa na,
The Industry PR
John Kiandika

Share this:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

 
Back To Top
Copyright © 2014 MOUNT KILI NEWS. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates