Ticker

6/recent/ticker-posts

CCM MWANGA WAJIVUNIA KUTOVURUGWA NA WAPINZANI

 Kaimu katibu mkuu wa UVCCM taifa Shaka Hamdu Shaka akiwa anapanda mti  nje ya ofisi ya CCM wilaya ya Mwanga

 kaimu katibu mkuu UVCCM taifa akiwa anaongea na wananchi wa kata ya Kileo iliopo ndani ya Wilaya ya Mwanga

 kaimu katibu mkuu UVCCM taifa Shaka Hamdu Shaka akiwa anamkabidhi  kiongozi wa timu ya Kileo  jezi  ambazo UVCCM  mkoa wa Kilimanjaro waliaidi timu
 Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa kilimanjaro Juma Raibu Juma akiwa anapanda mti wa ukumbusho  nje ya ofisi ya CCM wilaya ya mwanga




 Shaka akiongea na wanachama wa CCM wilaya ya Mwanga hii leo
Na Woinde Shizza, Mwanga
Wanachama wa chama  Mpinduzi wilaya ya Mwanga mkoa kiliimanjaro kimesema pamoja na kupita kimbunga cha siasa za maji taka zilizosheheni   ushabiki , ubabaishaji  na hujuma wana  ccm wilayani hiyo   wamebaki  wamoja bila kuyumbishwa na wanasiasa wasaka madaraka kwa njia za hila na fedha .
Pia wanachama hao  wamesema kuwa  wale wote ambao  walifuata siasa za ushabiki kwa  kushabikia mambo  bila kupima uzani wa siasa na ubora wa kila chama  sasa hivi  wako katika dimbwi la majuto na fedheha  kwani wameshaona hasara za kuhama chama hicho.
Hayo yasemwa leo  na Katibu wa CCM  wilaya ya Mwanga  Mkoa kilimanjaro Mwanaidi Hussein Misha wakati akitoa neno la  shukran mara baada ya Kaimu katibu Mkuu UVCCM Shaka  Hamdu Shaka kuzungumza na viongozi wa vijiji na kata pamoja na wanachama wa chama hicho wilayani Mwanga mkoani hapa.
Mbisha alisema umadhubuti waCCM  usichukukiwe kama janbo jepesi na rahisi badala yake viongozi wa upinzani na wanachama wanaoshabikia vyama hivyo wakubali ukweli kuwa ccm ni zaidi mbuyu mnene wa karene ulio imara.
Alisema CCM iliioachwa na marehemu baba Taifa Mwalimu julius Nyerere , mzee Abeid Karume., mzee Rashid Kawawa na mzee Thabit Kombo itabaki bkuwa kimbilio na tarajio la wananchi katika kufanikisha masuala yao kisiasa, kijamii na kiuchumi.
"Shaka nimekuwa nikikusikiasikia tu na kukusoma katika vyombo vya habari,wewe bado kijana mdogo ila unatosha kubeba hata dhamana kubwa., endelea mungu atakisaidia uthibitishwe kuwa Katibu mkuu "alisema mbisha.
Akizungumzia kimbunga na bhamkani za kisiasa wakati qa uchaguzi miuu, katibu hiyo wa wilaya aliwasifu sana wanachama wa CCM , viongozi wastaafu, wazee, wanawake na vijana  kwa kushikamana pia kupambana toka mwanzo  hadi mwisho..
"Mayowe na kelele za wapinzani zimepotea angani, sasa wote  kimya, wanatamani kurejea ccm wanaona aibu,hapana waambieni tu waje chama kitawapokea,hata waliotaka urais kama wamejirudi waje nyumbani kwao "alisema Mbisha.
Awali Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa kilimanjaro Juma Raibu Juma aliisifu wilaya ya mwanga kwa kuendelea kuwatoa mchanga wa macho kwa kuilinda jimbo hilo lisichukuliwe na upinzani.
Raibu alisema heshima ya wana mwanga kwa ccm itaendelea kuenziwa na kukumbukwa kika wakati kwasababu ni watu jasiri wenye msimamo thabiti.
"Unapokuwa vitani halafu wapiganaji wako wakakataa katakata kupokeabhongo toka kwa maadui, wakasema hatutaki na hatujunaki chochote , hao nibwazalendo na waakinifu kama wana mwabga"alisema Juma
Hata hivyo Mwenywkiti huyo wa UVCCM  mkoa wa Kilimanjaro alimpongeza   Kaimu katibu mkuu shaka kwa uthubutu wake wa kupania kurudisha heshima na hadhi ya UVCCM iliyokuwa  inapotea
Shaka anaendekea na ziara yake katika wilaya ya Same ambako atajitimisha katika mkoa kilimanjaro kabla ya kuanza mkoani Tanga kwa siku sita baadae Mikao ya Manyara,Kilimanjaro nq Arusha  itafanya majumuisho ya pamoja mkoani mkoani hapa.

Post a Comment

0 Comments