Ticker

6/recent/ticker-posts

HAMAD AANZA MBIO NA WAKULIMA WA ZANZIBAR


Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
Waziri wa Kilimo, Maliasil, Mifugo na Uvuvi Hamad Rashid Mohamed  amekutana na wakulima  wa kilimo  cha mwani kwa lengo la kusikiliza na kubaini  sababu ya kushuka  bei ya zao hilo viswani humu.
Hamad aliwatembekea wavuvi hao katika Wilaya ya Kati Mmkoa wa Kusoni Unguja ili kusikiliza malalamiko ya wakulima  kufuatia kushuka  bei ya zao  hilo toka shilingi 600/700  hadi 400/300 .
Mwani ni la pili kwa wingi na la tatu katika kuchangia  pato la Taifa visiwani humu.
Takriban wakulima wanaofikiri 23, 500 sawa na asilimia 90% wengi wakiwa wanawake ,  huzalisha  wastani wa  tani 16500 kila mwaka visiwani zanzibar .
Waziri Hamad, aliwaahidi wa kulima hao kuwa ifikapo jumatano serikali ya Mapinduzi Zanzbar itatatangaza kiwango cha bei elekezi ya zao la mwani.
Alisema pia smz itaeleza jinsi ya ushiriki wa shirika ZSTC katika ununuzi wa mwani pale ambapo sekta binafsi inaposhindwa kununua au kupanga bei isio na tija wala faida kwa wakulima.
"Nitazungumza na  wawekezaji kwa lengo la kuanzisha viwanda vya kuusarifu mwani wenye matumizi zaidi ya nane( 8 ) , upo uwezekano wa kuongeza thamani, serikali  atajitahidi kuangalia uwezekano wa kupumguza gharama za uzalishaji " alisema Hamad
Hata hivyo mara baada ya maelezo hayo toka kwa Waziri huyo  dhamana  wakulima wa zao hilo  walionyesha kufurahia msimamo  wa serikali na kujengeka matumaini  mapya chini ya Wizara  kilimo, mifugo, maliasili na uvuvi.
Wakulima walielezea matumaini yao wakisema ni fahari  kuona Waziri mhusika  wa Serikaii akiwa  kiongozi wa kwanza kutembelea   maeneo ya bahari ambako wakulima wa zao hilo hufanya ukulima na  uzalishaji.

Post a Comment

0 Comments