Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
Waziri wa Kilimo, Maliasil, Mifugo na Uvuvi Hamad Rashid Mohamed
amekutana na wakulima wa kilimo cha mwani kwa lengo la kusikiliza na
kubaini sababu ya kushuka bei ya zao hilo viswani humu.
Hamad aliwatembekea wavuvi hao katika Wilaya ya Kati Mmkoa wa Kusoni
Unguja ili kusikiliza malalamiko ya wakulima kufuatia kushuka bei ya
zao hilo toka shilingi 600/700 hadi 400/300 .
Mwani ni la pili kwa wingi na la tatu katika kuchangia pato la Taifa visiwani humu.
Takriban wakulima wanaofikiri 23, 500 sawa na asilimia 90% wengi wakiwa
wanawake , huzalisha wastani wa tani 16500 kila mwaka visiwani
zanzibar .
Waziri Hamad, aliwaahidi wa kulima hao kuwa ifikapo jumatano serikali ya
Mapinduzi Zanzbar itatatangaza kiwango cha bei elekezi ya zao la mwani.
Alisema pia smz itaeleza jinsi ya ushiriki wa shirika ZSTC katika
ununuzi wa mwani pale ambapo sekta binafsi inaposhindwa kununua au
kupanga bei isio na tija wala faida kwa wakulima.
"Nitazungumza na wawekezaji kwa lengo la kuanzisha viwanda vya
kuusarifu mwani wenye matumizi zaidi ya nane( 8 ) , upo uwezekano wa
kuongeza thamani, serikali atajitahidi kuangalia uwezekano wa kupumguza
gharama za uzalishaji " alisema Hamad
Hata hivyo mara baada ya maelezo hayo toka kwa Waziri huyo dhamana
wakulima wa zao hilo walionyesha kufurahia msimamo wa serikali na
kujengeka matumaini mapya chini ya Wizara kilimo, mifugo, maliasili na
uvuvi.
Wakulima walielezea matumaini yao wakisema ni fahari kuona Waziri
mhusika wa Serikaii akiwa kiongozi wa kwanza kutembelea maeneo ya
bahari ambako wakulima wa zao hilo hufanya ukulima na uzalishaji.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia