Ticker

6/recent/ticker-posts

ASILIMIA 93.3% WAPATA VITAMBULISHO VYA TAIFA (NIDA ) MKOANI ARUSHA



Image result for serikali mkoani arusha ofisini kwake Katibu Tawala wa mkoa Huo Richard Kwitega
Mamlaka ya usajili wa vitambulisho vya Taifa(NIDA) imekamilisha zoezi kwa asilimia 93.3% kuandikisha na kutoa vitambulisho kwa wafayakazi wa sekta ya umma mkoani Arusha ambapo jumla ya wafanyakazi 26,992 toka kada mbali mbali serikalini walitarajiwa kuandikishwa katika zoezi hili ni 25,278 ndio wameandikishwa na kupewa vitambulisho huku wengine wakishindwa kujiandikishwa kutokana na sababu mbalimbali
Akisoma Taarifa hiyo wakati akipokea vitambulisho hivyo vya watumishi wa serikali mkoani hapa ofisini kwake Katibu Tawala wa mkoa Huo Richard Kwitega alisema kuwa changamoto kubwa waliokumbana nayo ni kuchelewa kujitokeza kwa baadhi ya watumishi ambao walikuwa wakichanganya zoezi hilo na zoezi la kuhakiki vyetu.
Kwitega alisema kuwa pamoja na changamoto hiyo bado zoezi hilo halikuweza kuathirika ambapo aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika kujiandikisha kwenye zoezi linalotarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi huu au mwanzoni mwa mwezi wa Januari,
Alisema kuwa jumla ya makadirio ya wananchi wanatarajiwa kuandikishwa kwenye zoezi hilo kwa kuchukuliwa taarifa zao ni 975,988 ambap kwa siku wanatarajia kuandikiasha watu 50 kwa mwandikishaji moja ili kupunguza misongamano.
Akavitaka vyombo vya habari,viongozi wa umma, kuendelea kutoa elimu kwa umma juu ya umuhimu wa vitambulisho vya taifa ili siku ya kuanza kwa zoezi hilo waweze kujitokeza kwa wingi nakuweza kutumia fursa hiyo.
Alisema ushirikiano wa serikali na Nida ndio umeweza kufanikisha zoezi hilo kwa watumishi wa umma ambapo ambao hawajajiandikisha walitokana na wengine kuwa masomoni na wagonjwa ambapo kwa sasa watawafata huko walipo ili waweze kuwaandikisha wote.
Nae Afisa usajili wa Nida mkoa wa Arusha Julieth Raymond Mwacha alisema kuwa zoezi hilo limeenda vizuri na kuwataka wananchi kusubiria zamu yao kwa kutoa taarifa zao sahihi za kuomba kitambulisho cha taifa kwani zoezi hilo hivi karibu litaingia kwa wananchi wa mkoa mzima.
Alisema kuwa zoezi hilo likikamilika litaisaida serikali hata kwenye takwimu zake mbali mbali kwani taarifa zimewekwa kwenye kanzidatam na kukoa fedha ambazo zingetumika katika mazoezi mengine ya kitakwimu.

Post a Comment

0 Comments