Ticker

6/recent/ticker-posts

KESI INAYOMKABILI MBUNGE WA JIMBO LA ARUSHA MJINI GODBLESS LEMA NA MKE WAKE YA KUMTUMIA UJUMBE WA KUMTUKANA MKUU WA MKOA WA ARUSHA KUSIKILIZWA TENA FEBRUARY TATU MWAKA HUU

Image result for picha ya lema na mkewe




Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema na mkewe Neema Lema wamefikishwa katika  mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Arusha kusomewa mashtaka yanayowakibili katika kesi namba 351 ambapo wanatuhumiwa kutuma meseji yenye ujumbe wa kumtukuna mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Mashaka Gambo

Wakili wa upande wa mashtaka Alice Mtenga amewataja mashahidi watano wakiongozwa na mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo ambao watatoa ushahidi katika kesi hii

Hata hivyo mawakili upande wa utetezi wakiongozwa na John Malya umetoa notisi ya pingamizi la awali la mdomo kuwa hati ya mashitaka ina mapungufu kwa hiyo baadae wataiomba mahakama itupilie mbali hati hiyo.

Hakimu anayesikiliza shitaka hili Nestory Barro ameiahrisha kesi hiyo hadi tareh 3 mwezi februari mwaka huu

Post a Comment

0 Comments