Ticker

6/recent/ticker-posts

PINGAMIZI LA JAMUHURI LAMRUDISHA LEMA MAGEREZA

 
Na Woinde Shizza,Arusha
Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema amelazimika kurudishwa tena  gerezani mara baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Arusha kushindwa kutoa uamuzi baada ya upande wa Jamhuri kukata rufaa kwenda Mahakama ya Rufani kupinga mbunge huyo kupewa dhamana.

Jaji wa Mahakama kuu ya Arusha aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo Salma Magimbi ameshindwa  kutoa maamuzi kutokana na upande wa Jamhuri kukata rufaa ya mahakama kuu ya Rufaa kupinga dhamana dhidi ya Mh. Lema.

Jaji huyo amesema hana mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo kutokana na uamuzi huo; hivyo kusababisha mbunge Lema kurudishwa tena mahabusu.

Kwa upande wa Wakili mtetezi wa Mbunge Lema John Malya akielezea mwenendo wa kesi hiyo kwa niaba ya mawakili wenzake amesema wamesikitishwa na uamuzi uliotolewa mahakamani leo kwani Jamhuri wangepaswa kutoa uamuzi wa dhamana na siyo kukata rufaa juu ya rufaa.

Amesema jambo hilo linalobishaniwa na upande wa Jamhuri lipo wazi na kwamba wanajipanga kwenda katika mahakama kuu ya rufaa kabla yao ili shauri hilo liweze kusikilizwa na mteja wao amekubaliana nao.

Mbunge huyo amerudishwa tena Rumande hadi hapo kesi hiyo itakaposikilizwa tena ambapo mpaka sasa amefikisha siku 61 akiwa mahabusu.

Post a Comment

0 Comments