Ticker

6/recent/ticker-posts

MWIJAGE:SERIKALI HAITAACHA KUHIMIZA UJENZI WA VIWANDA


Na.Mwandishi Wetu,Chalinze
Serikali imesema haitasita kuaendelea kuhimiza na kuvutia wawekezaji waaminifu,  wenye mipango, dhamira na mikakati ya ujenzi wa viwanda kwa nia ya kutanua wigo wa ajira na kukuza  maendeleo ya kiuchumi.

Msimamo huo.umetolewa jana na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage wakati akipongeza  jitihada zinazofanywa na mwekezaji wa kampuni TwyFord Tanzania Cereramics katika  ujenzi wa kiwanda cha kutengeneza vigae "Tiles" kilichopo Kijiji cha Pingo, Chalinze Mkoani Pwani.

Waziri Mwijage alisema hayo mara baada ya kutembelea na kukagua maendeleo ya awali ya eneo litakalojengwa kiwanda cha kutengeneza vigae  kitakachozalisha  ajira kwa watanzania zaidi ya elfu mbili katika mfumo rasmi na ajira elfu nne zisizo rasmi.

“Kiwanda hiki kikikamilika kitasidia sio tu kutoa ajira lakini pia kitawafanya watanzania kununua na kuuza bidhaa zinazotengenezwa nyumbni badala kuangiza kila kitu kununua  nje” Alisema Mwijage.
Waziri huyo dhamana wa viwanda  alisema, bidhaa hizo pia zitauzwa katika nchi jirani kama Zambia, Malawi,  DRC, Rwanda, Burundi, Uganda na Jamhuri ya watu wa Afrika Kati pia kusafirishwa nje ya bara la Afrika .

Aidha Waziri Mwijage alisema kuwa  kiwanda hicho kitumike vizuri hukubakitoa wito kwa watanzania kutumia fursa zitakazopatikana katika mradi huo zitumike kwa faida ya kila mmoja.
“Serikali ya kijiji itambue maeneo yake ili kusaidia kuharakisha maendeleo ya eneo hili mahali ambapo kiwanda kinafanya shughuli zake”Alisema Mwijage.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete, alisema  ujenzi  wa kiwanda hicho kipo katika hatua ya mwanzo ya Ujenzi na kinataraji kukamilika julai mwaka  na kufunguliwa rasmi Agosti  mwaka huu.

Ridhiwani alisema  kiwanda hicho kitasaidia kuufungua mji wa Chalinze na kufanya uwe mji wa viwanda na biashara hivyo kutaanza kufunguka kwa fursa za kiuchumi na kupanua mji huo  sekta ya viawanda katika juhudi za kuunga mkono  serikali ya awamu ya tano.

“Ujenzi wa kiwanda hiki ni alama chanya ya jinsi serikali ya awamu ya tano ilivyojidhatiti kufungua fursa za viwanda katika nchi yetu.Wananchi wa Chalinze na mkoa wa Pwani nawaasa na kuwataka waendelee kujipanga kwa nia ys kujenga viwanda ili fursa nyingi zaidi.”Alisema Ridhiwani

Mbunge huyo wa chalinze alimshukuru mwekezaji wa kiwanda hicho  kwa kukubali kusaidia kumalizia ujenzi wa shule ya sekondari ya kata ya Pera na kituo cha afya katika kata hiyo.

“licha ya kukubali kusaidia  ujenzi wa huo lakini pia fursa nyingine watu watapata  nafasi ya kuuza mali ghafi zinazotumika kutengeza  vigae  ambapo tunatarajia asilimia 90 malighafi hizo zitatoka hapa kwetu katika  mikoa ya jirani”.alisema Ridhiwan.

Post a Comment

0 Comments