Ticker

6/recent/ticker-posts

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji akutana na mamlaka za udhibiti na utoaji leseni.


Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage akizungumza katika kikao cha wadau kutoka taasisi mbalimbali waliokutana na kamati ya marekebisho ya wepesi wa kufanya shughuli nchini, kushoto kwa waziri ni Katibu Mkuu biashara na uwekezaji Mhe. Prof. Adolf Mkenda, Mwenyekiti wa kamati ya kuboresha mazingira ya biashara Dkt. John Mduma, kulia kwa waziri ni Katibu tawala Kibaha Ndg. Anatory Mhango.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage akizungumza katika kikao cha wadau kutoka taasisi mbalimbali waliokutana na kamati ya kuboresha mazingira ya kufanya biashara nchini katika ukumbi wa kituo cha utafiti wa miwa na muhogo mjini Kibaha.
Katibu Mkuu Biashara na Uwekezaji, Mhe. Prof. Adolf Mkenda akizungumza katika kikao cha wadau kutoka taasisi mbalimbali waliokutana na kamati ya kuboresha mazingira ya kufanya biashara nchini katika ukumbi wa kituo cha utafiti wa miwa na muhogo mjini Kibaha.
Wadau kutoka taasisi mbalimbali za serikali waliokutana na kamati ya kuboresha mazingira ya kufanya biashara nchini katika ukumbi wa kituo cha utafiti wa miwa na muhogo mjini Kibaha.
Wadau kutoka taasisi mbalimbali waliokutana na kamati ya kuboresha mazingira ya kufanya biashara nchini katika ukumbi wa kituo cha utafiti wa miwa na muhogo mjini Kibaha.
Wadau kutoka taasisi mbalimbali waliokutana na kamati ya kuboresha mazingira ya kufanya biashara nchini katika ukumbi wa kituo cha utafiti wa miwa na muhogo mjini Kibaha.

………………

Waziri wa viwanda, Biashara na uwekezaji akutana na kamati ya kuboresha ya mazingira ya biashara ambayo inahusisha wataalamu kutoka sekta mbalimbali katika wizara zote, TBS, EWURA, SUMATRA, TRA, OSHA, WMA, NCC, n.k na kujadili changamoto mbalimbali ambazo ni vikwazo katika wepesi wa kufanya shughuli.

Waziri amehimiza wataalamu hawa kujadili changamoto na kutoa mapendekezo ya namna ya kuondoa kero hizo ili kuboresha urahisi wa kufanya shughuli nchini Tanzania na kuvutia wawekezaji.

Waziri amehimiza ulipaji wa kodi ili kuleta maendeleo ya watu, kwani kwa takwimu Tanzania ni ya 154 kati ya nchi 190 hivyo kuhimiza wafanyabiashara wote kuwa na Tin namba na pia kulipa kodi.

Mkutano huu umefanyika jumamosi tarehe 21/1/2017 ukumbi wa kituo cha utafiti wa miwa na muhogo mjini Kibaha.

Post a Comment

0 Comments