Ticker

6/recent/ticker-posts

JESHI LA POLISI LATEKETEZA MAGUNIA 58 YA BANGI

 kamanda wa polisi mkoani Arusha  naibu kamishna wa polisi Charles mkumbo akiongea na waandishi wa habari hii leo juu ya uteketezaji wa magunia ya bangi ,pembeni ni mkuu wa kitengo cha kupambana  na kuzuia  madawa ya kulevya nchini  kamishina  msaidizi mwandamizi  wa polisi (SACP) Mihayo Msikhela



Na Woinde Shizza,Arusha
Jeshi la polisi mkoani hapa kwa kushirikiana na tume ya kuratibu na   kuthibiti dawa  za kulevya nchini limeteketeza magunia 58 ya bangi,mbegu za  bangi  kg 210  huku hekari 19 zilizooteshwa miche ya bangi  zikiwa zimeharibiwa  .
Hayo yamebainishwa jana na kamanda wa polisi mkoani Arusha  naibu kamishna wa polisi Charles mkumbo wakati akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake ambapo alisema kuwa kuteketeza kwa madawa haya ya kulevywa kumefanyika kutokana na operationi  ya siku mbili .
Alisema kuwa operesheni ya kwanza ilofanyika january 10  siku ya jumanne kuanzia muda wa saa 11.00 alfajiri katika eneo la kijiji cha kisimiri juu ndani ya kata ya uwiro tarafa ya kingori na kufanikiwa kupata  magunia 31 pamoja na mbegu kilogramu 210 ambazo zote ziliteketezwa na moto ,pamoja na hekari 19 zilizooteshwa miche ya bhangi ambazo ziliaribiwa zote.
Aliongeza kuwa operationi hiyo iliendelea tena siku ya alhamisi january 12 kuanzia muda wa saa 11.00 alfajiri hadi saa saba mchana katika eneo la kijiji cha Engalaon kata Mwandeti tarafa ya Muklati ambapo walikamata jumla ya magunia 27 ya bangi na kuyateketeza na moto na kuharibu jumla ya hekari 12 zilizooteshwa mmea wa bhangi .
Mkumbo alisema kuwa jeshi la polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama linaendelea na operationi hii hasa ya kuaribu mimea ya bangi mara kwa mara hasa katika cha mvua hali ambayo itasaidia kuthibiti kilimo hicho.
Aidha pia jeshi la polisi linawaonya viongozi wa maeneo yanayohusika na kilimo cha bangi kuacha mara moja kuwaunga mkono wakazi wa maeneo hayo kwani matukio hayo yanafanywa kwa uwazi bila wao kuchukua hatua yeyote  ,wanapaswa watambue kwamba wao ni walinzi wa maeneo yao ,na kuwasihi viongozi washirikiane kwa pamoja kutokomeza kilimo hicho cha bhangi ambayo inaleta madhara makubwa kwa jamii.
  kwa upande wake mkuu wa kitengo cha kupambana  na kuzuia  madawa ya kulevya nchini  kamishina  msaidizi mwandamizi  wa polisi (SACP) Mihayo Msikhela alisema kuwa mikoa ambayo inaongoza na kupatikana kwa zao la bangi ni Tarime ,Morogoro , Arusha pamoja na Kilimanjaro  lakini kwa sasa viongozi waliopo katika sehemu hizo wanajitaidi sana kuthibiti ulimwaji wa mazao hayo ya bangi  huku akichukuwa muda huo kumpongeza mkuu wa wilaya ya Arumeru kwa kupiga vita  ulimwanyi wa bangi pamoja na mkuu wa wilaya ya Tarime jinsi wanavyojitaidi kuthibiti ulimwaji huo wa bangi mpaka kufikia sehemu ya kuwaweza viongozi wa vijiji hivyo ndani kutokana na kusimamia ulimwaji wa zao hilo ambalo limepigwa marufuku hapa nchini
Aidha alisema kuwa kwakuwa tatizo hili limekuwa kama likijirudia  wanampango wa kuboresha sheria za uthibiti  ikiwa ni pamoja na kuweka sheria kali zitakazo wabana wale ambao wanatumia ,wanauza pamoja na wanao lima madawa haya ya kulevya hapa nchini .


Post a Comment

0 Comments