Ticker

6/recent/ticker-posts

WAISLAMU WATAKIWA KUSOMESHA WATOTO WA ILI KUENDANA NA NYAKATI ZILIZOPO




Waislamu wametakiwa kusomesha watoto wao ili kuweza kuendana na mifumo ya kielimu kwa nyakati zilizopo na zijazo kwani vijana wa sasa wamekuwa na ulimwengu wa haraka haraka na umekuwa unabadilisha lugha kila mara
Kauli hiyo imetolewa na mjumbe wa baraza la ulamaa bakwata taifa sheikh Hassan chizenga wakati akizungumza na waislamu kwenye uzinduzi wa ujenzi wa jengo la chuo cha Al Azhar na mgeni Rasmi kuwa mkuu wa wilaya ya Arusha Fabian Daqarro
Sheikh Chizenga alisema kuwa elimu ni kitu muhimu katika maisha na chuo hicho kitakapokamilika watoto wetu watafundishwa kuijua dunia yao na akhera yao itakayosaidia kuwa waadilifu katika utumishi wa umma na mbele ya muumba wao kama mafundisho ya mtume Muhammad s.w.a.
Alisema kuwa Kuijenga Tanzania yenye maadili mema amani na mshikamano inahitaji nguvu ya ziada ya kuaandaa watoto wetu katika malezi mema ya kiroho na kidunia yatakayowasaidia kupata fedha za halali na watoto wa halali ilikuweza kuendesha maisha ya halali na hatimae watoto hawa kuwa waadilifu kwenye taifa lao.
“Tutambue kuwa sisi tunaishi kwenye ulimwengu wenye kugeuka tabia kila mara na vijana wetu wanazaliwa kwenye ulimwengu wa haraka haraka hivyo yatupasa kuwapa elimu ya utambuzi itakayowasaidia kuishi maisha ya halali na kuja kulisaidia taifa lao siku za usoni wakiwa waadilifu”alisisitiza Sheikh Chizenga
Aidha mgeni rasmi mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo  kwa niaba yake Mkuu wa Wilaya ya Arusha Gabriel Daqarro alisema kuwa taasisi za dini zimekuwa na mchango mkubwa kwa serikali hususani katika masuala mbali mbali ya kijamii ikiwemo elimu na Afya.
Daqarro alisema kuwa Taifa linahitaji kuwa na amani na mshikamano utakaosaidia kuendelea kuwa darasa kwa mataifa yanaotuzungika na kuishi bila chuki na mtu unaetofautiana nae mawazo kwa kukaa na kujadiliana nae tofauti zenu bila munkari.
Alisema kuwa viongozi wa serikali wanawategemea viongozi wa dini kuwajenga kiimani waumini wao kujua umuhimu wa mafundisho ya kuitunza amani sanjari na uadilifu utakalolisaidia taifa eltu kuendelea kuwa na amani na mshikamano kama hapo mwanzo wakati wa waasisi wetu wa taifa hili.
“Amani ni kila kitu amani ni sawa na Oxygen tuienzi kwani viongozi wa dini wamekuwa washiriki wakubwa wa kuleta maendeleo katika nchi yetu kama nyinyi leo mnavyoonyesha katika chuo hichi cha Al Azhar”alisema Daqarro.
Nae sheikh wa mkoa wa Arusha Shaban Jumaa alisema jengo hilo litakapokamilika litakuwa na ghorofa 14 na litagharimu zaidi ya billion 12 na litajengwa kwa awamu tatu likiwa na lengo la kuboresha elimu ya dini na sekula pamoja na hospitali,hosteli,shule ya awali,msingi hadi ngazi ya chuo.
Sheikh Shaban alisema kuwa ujenzi wa chuo hicho utawashirikisha wanaarusha wote kuchangia ujenzi wake,ambapo ukikamilika utazalisha vijana wenye maadili ya kulitumikia taifa kwa uadilifu na uzalendo na uchungu kwa wananchi wanyonge.
“Nafikiri amani imezungumzwa sana faida zake na hasara zake tuviangalie vyombo tunavyoviongoza kwa jicho la utofauti kwa kuangalia mema ya mwenzako na kuyazungumza huku mabaya mkikaa chini na kuyajadili mtafika kwenye kuheshimiana nawasihi sana kuzungumza mema kuliko mabaya”alisema sheikh Jumaaa

Post a Comment

0 Comments