Ticker

6/recent/ticker-posts

WATANZANIA SAIDIENI JAMII YA WATU WASIOJIWEZA


 Nabii mkuu mheshimiwa Dr Geordavie akiombea  bajeti mbalimbali  za waumini walizoziletwa kwa ajili ya kutolewa neno la unabii hiii leo


Na Woinde Shizza,Arusha.



Watanzania nchini wametakiwa kusaidia Jamii ya watu wasiojiweza ikiwemo walemavu,watoto yatima pamoja na wazee ili waweze kupata mahitaji yao na kuondokana na umasikini uliokithiri.



Hayo yameelezwa na Baadhi ya Wananchi waishio katika kata ya Kisongo mkoani Arusha ambapo walisema kuwa jamii ya wahitaji imekua ikiishi katika mazingira magumu hivyo ni jukumu la kila Mtanzania kuhakikisha kuwa anawasaidia jamii hiyo.

"katika jamii kuna watu wengi wakiwemo watoto wanatoto na watu wasio jiweza ambao wanakaa katika mazingira magumu mno  hivyo ni wajibu wetu sisi kuwasiaidia wale ambao awajiwezi ,mtu ukiwa na uwezao kidogo unatakiwa ujijengee tabia ya kuwasiaida hawa wasio jiweza"alisema Sekela Tondolo



Kwa upande wake Mkazi mwingine wa kata ya  Kisongo Wiliam James Alisema kuwa  jamii ya wasiojiweza imekua ikisahaulika mara kwa mara hivyo ni jukumu la kila Mwananchi kuhakikisha kuwa anafanya kitu kwa ajili ya jamii yake kitakacholeta mchango ambao ni chanya na kuwawezesha kukabiliana na changamoto wanazokutana nazo kimaisha.



Kwa upande wake Mheshimiwa Nabii Mkuu Dr. Geor  Davie  wa Huduma ya Ngurumo ya Upako  katika ibada ya makusanyo ya vitu na fedha kwa ajili ya kuwasaidia wahitaji alisema kuwa taasisi za dini hazina budi kujikita katika kuwasaidia wahitaji na wasiojiweza ili kuwa na taifa imara na endelevu .

"ni wajibu wa taasisi za kidini  ,makampuni mbalimbali , hata watu binafsi ambao wanauwezo kuweza kusaidia watu hawa wenye mahitaji na walae wasio jiweza ili nao wajisikie vyema na kuona nao  ni sehemu ya watu kama wengine "alisema  Geor  Davie



Huduma hiyo inautaratibu endelevu wa kila mwaka wa kupeleka mahitaji kwa wato wasiojiweza pamoja na kuwawezesha kiuchumi kaya zilizoathiriwa na umasikini kwa kiasi kikubwa.

Post a Comment

0 Comments