Ticker

6/recent/ticker-posts

JESHI LA POLISI ARUSHA:WATAKAOCHOMA MATAIRI,FAINI MILIONI NNE,MADEREVA WALEVI KUKAMATWA NA KUNYANG'ANYWA LESENI,WAZAZ I/WALEZI WATAKAOWAACHA WATOTO WAKAZURURA OVYO KUSHTAKIWA,WENYE VIBALI VYA KUFYATUA FATAKI KUTUMIA DAKIKA TATU TU

Image result for kamanda wa polisi
charles mkumbo


Jeshi la polisi mkoani Arusha limesema kuwa katika kusheherekea mwaka mpya ,kumekuwa na kasumba kwa baadhi ya watu kufanya matukio ya kuhatarisha usalama kwa kuchoma matairi,kupanga mawe barabarani,na hata kuwarushia mawe askari pindi wanapothibiti matukio hayo,haswa maeneo ya majengo,kwa mrombo,kwa mrefu huku wengine wakitumia mwanya huo kufanya uhalifu.


Kwa wale watakaochoma na watakaokamatwa wamechoma matairi barabarani,wakumbuke kwamba watashtakiwa kwa sheria za Tanroad, ambapo watatakiwa kulipa faini isiyopungua milioni nne


Lakini pia baadhi ya madereva huwa wanatumia vilevi kupita kiasi katika majumba ya starehe inapofika saa 00:00 usiku unapoanza mwaka mpya huwa wanashangilia kwa kuendesha vyombo vyao kwa mwendo kasi na kupiga honi mitaani huku wakiwa wamepakia watu kwa kuwaning’iniza milangoni kama njia ya kuonyesha furaha zao.


Uzowefu unaonyesha kwamba maeneo ya sakina mpaka kwa iddi baadhi ya madereva wanatuamia magari aina ya altezana Subaru huwa wanafanya maonyesho kwa kuendesha mwendo kasi vyombo hivyo huku vikitoa sauti kama risasi.


Kwa upande wa wamiliki wa bar wazingatie masharti ya leseni zao ambazo zinaonyesha muda halisi wa kufunga na wasiwe na tama ya kuendelea kupata pesa baada ya kuona wateja wengi katika biashara ,hali kadhalika wamiliki wa kumbi na maeneo mengine ya starehe wanatakiwa kuzingatia usalama katika maeneo yao hasa kwa kuweka wasimamizi na kutojaza watu kupita kiasi.


Aidha wazazi na walezi tunawakumbusha pamoja na kusheherekea mwaka mpya wa 2017 wasisahau majukumu yao ya kuwa makini na watoto kwa kutowaacha peke yao na hata kutoacha mtu yeyote katika majumba ili kuondokana na matukio yanayoweza kuepukika sambamba na kuangalia watoto wao katika maeneo ya round about hasa kijenge mnara wa mwenge,wasizagae barabarani


Jeshi la polisi linatoa onyo kwa baadhi ya watu watakaofanya makosa yaliyoorodheswa hapo juu ,tutawakamata na kuwachukulia hatua za kisheria wawe wahalifu ,wamiliki wa bar na kumbi nyingine za starehe pamoja na wazazi au walezi na madereva walevi ambao pia watapima na ikithibitika wamevuka viwango tutawafungia leseni.


Kwa upande wa waaliomba vibali vya kufyatua fataki ,watatakiwa watumie dakika tatu na wote kwa pamoja watatakiwa kufyatua saa 00:00 na pia hawataruhusiwa kufyatua katika makazi ya watu.


Tutahakikisha nyumba zote za ibada ,kumbi za starehe na maeneo mengine kutakuwa na ulinzi wa kutosha ambapo askari watakuwa katika doroa za miguu na doria za magari kila kona ya jiji la Arusha na wilaya zote za mkoa huu ,hivyo waumini wa dini mbalimbali wasiwe na hofu pindi watakapokuwa wanaendelea na ibada.


Kama ilivyo kwa nyakati zote tunawaomba wananchi waendelee kushirikiana nasi katika kuwabaini na kuwafichua wahalifu na uhalifu ili kuimarisha amani na utulivu uliopo.


Mwisho tunatoa shukrani za dhati kwa vyombo vya habari radio,magazeti,blogs,televisheni,kwa  ushirikiano mkubwa mnaotoa kwa jeshi la polisi mkoa wa Arusha kwa kuwa mbele katika kufichua, kuelimisha,na kuhabarisha umma juu ya uhalifu.


Jeshi la polisi mkoa wa Arusha tunawatakia heri ya mwaka mpya wa 2017 wakazi wote wa Arusha .


       IMETOLEWA NA KAMANDA WA POLISI MKOA WA ARUSHA

                         NAIBU KAMISHANA WA POLISI

                          (DCP)CHARLES MKUMBO

                                  TAREHE 29/12/2016

Post a Comment

0 Comments