SAME YAENDELEA KUPUNGUZIA WANANACHI MZIGO AMBAPO DC SAME AMEPOKEA MADARASA NA MRADI WA MAJI




Mkuu wa wilaya ya Same Bi Rose Mary Senyamule kwa niaba ya serikali amepokea  madarasa 6, ofisi za walimu, vyoo Na nyumba za walimu na mradi wa Maji kwa ajili ya wananchi ambapo ni ushirikiano wa masista wa Grail, Joy of faith Na Korea Hope Foundation. 
Bi Rose amesema madarasa hayo yamejengwa katika kitongoji cha Endevesi, kata ya Njoro, ambapo watu  inayoishi eneo ni jamii ya kifugaji
Amesema jamii hiyo ya Endevesi walikuwa  wakipata changamoto kubwa ambapo watoto walikuwa wakitembea umbali wa kilomita 5 kwa ajili ya kupata Elimu na kusababisha watoto wengi kukosa shule na wengi kuwa watoro.
" Shule tumejengewa, serikali tutahakikisha tunapanga walimu Na shule hii inaanza 2018. Wananchi hakikisheni mnawaleta watoto shuleni. Nasi tutawachukulia hatua wote watakaokuwa watoro." 
Hata hivyo amewashukuru wafadhali hao kwa kuunga mkono juhudi za Mh. Rais wa Tanzania katika kuhimiza elimu.

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

Previous Post Next Post